Thursday, October 23, 2014

KLABU BINGWA ULAYA ARSENAL, REAL MADRID ZAKANYAGAKANYAGA

 
Anderlecht akitupia goli la kwanza

 
  
Podolski akishangilia goli la ushindi

Katika ligi ya mabingwa barani Ulaya Liverpool imechabangwa nyumbani Anfield kwa mabao 3-0 kutoka kwa Real Madrid huku Mario Balotelli akiingia lawamani
Meneja wa mchezaji huyo mtukutu, Brendan Rodgers amemlaumu mshambuliaji huyo kwa kitendo chake cha kubadilishana Jezi na Pepe mara tu baada ya dakika 45 za kwanza.
Baadhi ya mashabiki wa jijini Dar es Salaam,Tanzania wamemtupia lawama mchezaji huyo ambaye pamoja na kununuliwa kwa pauni milioni 16 ameifungia Liverpool goli moja tu msimu huu.
Wakati huo huo Arsenal wamepata ushindi wa dakika za mwisho wa 2-1 baada ya Anderletch kuwakimbiza mchakamchaka kwa muda mrefu.
Mara baada ya mchezo huo nimezungumza na shabiki wa Arsenal ambaye anasema pamoja na ushindi walioupata lakini kuna haja ya Arsene Wenger kubadillika
Matokeo mengine ni Atletico Madrid wameifumua Malmo 5-0 na Olimpiakos imeichapa Juventus bao 1-0
Kwa upande wa michuano ya Uropa Ligi, leo Tottenham inakipiga na Asteras Tripolis, Inter Millan inakutana na St Etienne, Lille itamenyana na Evaton, wakati ambapo Viareale watacheza na FC Zurich
 
C.Ronaldo akishangilia baada ya kutupia goli la kwanza

Wachezaji wa Madrid wakimpongeza Benzema bada ya kutupia kambani bao la pili



Chukua hiyooooooooooo

 
ANDERLECHT 1-2 ARSENAL
 
LIVERPOOL 0-3 REAL MADRID


No comments:

Post a Comment