Thursday, December 1, 2011

Ubalozi wa Uingereza Iran wavamiwa,wafungwa wafanyakazi wapewa saa 48

Waandamanaji wakivamia ubalozi wa Uingereza mjini Tehran
waandamanaji wakivamia ubalozi wa Uingereza

Uingereza imeamuru kufungwa kwa ubalozi wake nchini Iran na kutaka wafanyakazi wa ubalozi huo wawe wameondoka katika muda wa saa 48.

Wandamanaji mjini Tehran 

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza, William Hague, ametangaza hatua ya kufunga ubalozi wake mjini Tehran ikiwa ni siku moja tangu waandamanaji wavamie ofisi za ubalozi wa Uingereza na maeneo mengine ya kibalozi nchini Iran.

 
Bendera ya Uingereza ikipigwa kiberiti
 
Uingereza pia imefunga ubalozi wa Iran mjini London na kuwafukuza maafisa wake wote.

Naye msemaje wa serikali ya Iran ameonya hatua ya Uingereza ya kufunga ubalozi wake nchini humo kuwa ni ya haraka mno, na amesema kuwa Iran itachukua hatua zaidi zinazostahili.

Nchi mbalimbali zimelaani mashambulio katika ofisi za Uingereza mjini Tehran.

Miongoni mwao ni Marekani na Ujerumani, huku nyingine zikitishia kufunga balozi zao nchini Iran.

Waandamanaji wakivunja geti la Ubalozi wa Uingereza.


Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani, Mark Toner, amesema hatua ya Uingereza na mataifa mengine inaashiria kuwa Iran inaendelea kutengwa.

''Hatua ya Tehran inaisababishia nchi hiyo kuendelea kutegwa zaidi na dunia. Ningependa kuongezea kuwa, kwa hakika Uingereza inawaondoa wafanyikazi wa ubalozi wake, Ujerumani na Uchina zimeamrishi mabalozi wake kurudi nyumbani'' Bwana Toner amesema.

Norway ilifunga Ubalozi wake kwa muda mjini Tehran kwa sababu za kiusalama, lakini bado haijawaondoa wafanyakazi wake.

SIKU YA UKIMWI DUNIANI December 1




Hizi ni takwimu zinazoonesha nchi ama maeneo yaliyoathiriwa kwa ukimwi zaidi Afrika kati ya mwaka 1999 mpaka mwaka 2001.



Hizi ndizo sababu zinazosababisha kuenea kwa Ukimwi katika jamii kwa kasi.

Tuesday, November 29, 2011

SIMBA MABINGWA VIJANA
















Vijana Simba wakishangilia ushindi

KILA mwaka hufanyika mashindano ya soka kwa timu za vijana chini ya miaka 20, lengo hasa likiwa kuibua vipaji na kuvikuza.
Programu hiyo ilibuniwa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kwa nia nzuri kabisa ya kuwajengea misingi bora wachezaji tangu wakiwa na umri mdogo ili baadae taifa lipate wanandinga makini kuunda timu ya taifa.
Hata hivyo, programu hiyo imeonekana kuzaa matunda baada ya kuibua wacheza wengi ambao wamepandishwa kuzichezea timu za wakubwa.
Baadhi ya klabu za Ligi Kuu, zimetangaza kuwapandisha chipukizi hao kwenye timu za wakubwa ili waweze kupata uzoefu na kukomaa kimashindano.
Ni msimu wa nne michuano hiyo inafanyika, lakini bado ni klabu chache zimeonyesha utayari kupokea wito huo pasipo kuelewa faida yake.
Mwaka huu zilishiriki timu 15 kutokana na ile ya Taifa kwa vijana U-17, Serengeti Boys kuongezwa kwa ajili ya kupata uzoefu wa mashindano.
Simba ambayo imeonyesha umakini na programu hiyo ya kukuza na kulea vipaji, ilitwaa ubingwa wa michuano hiyo kwa mara ya pili tangu mashindano hayo yaanzishwe mwaka 2007.
Iliifunga Azam FC kwa mikwaju ya penalti 6-5, katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa Karume Jumamosi iliyopita.
Kutokana na ushindi huo, ilijinyakulia kitita cha Sh1.5mil na Kikombe na kuvalishwa Medali za Dhahabu kama zawadi za bingwa wa michuano hiyo. Wakati Azam FC ikitwaa nafasi ya pili nakupatia Sh.1mil na Medali za Shaba.
Timu ya soka, Taifa Vijana U-17, Serengeti Boys ilishika nafasi ya tatu na kujitalia Sh500,000 na medali za fedha kwa kila mchezaji.
Mchezaji bora wa mashindano hayo alikuwa ni Ramadhan Singano wa Simba aliyejinyakulia kitita cha Sh400,000. Kipa bora ni Faishi Manula wa Azam aliyepata Sh300,000.
Mfungaji bora wa michuano hiyo alikuwa Simon Msuva wa Azam aliyepachika mabao sita na kujipatia Sh300,000.
Timu ambazo zilizoshiriki michuano hiyo ni Simba, Yanga, Azam, Mtibwa, Kagera, African Lyon, Toto African, Moro United, Polisi Tanzania, JKT Ruvu, Villa Squad, JKT Oljoro, Coastal Union, timu ya Taifa ya vijana U-17, Serengeti Boys na bingwa wa mwaka jana Ruvu Shooting.
Hata hivyo, wachezaji wa timu zote walilalamikia ratiba ya michuano hiyo kwa kucheza mechi tatu kwa siku ikiwa asubuhi, mchana na jioni.
Kwamba ratiba ilikuwa ya mechi za mfululizo na hakukuwa na sababu ya kucheza kufanya hivyo kwa kuwa muda ungalipo wa kuendesha mashindano hayo.
Vilevile kasoro nyingine ni viwanja uzoefu wa kucheza kwenye jua kali la nyasi bandia, ambazo watoto wengi walikuwa wakipata shida. Ni vema mechi hizo kuchezwa asubuhi ama jioni.
Tatizo lingine lililojitokeza ni kukosekana kwa huduma ya kwanza iliyosahihi. Ilibidi daktari wa Simba, Cosmas Kapinga kufanya kazi ya kuuguza wachezaji walioumia badala ya TFF ama wahusika kuwapatia huduma ya kwanza. Hata gari la wagonjwa kwa mchezaji ambaye angepata dharura halikuwepo.
Spoti Mikiki ilifanya mahojiano na makamu mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange kutoa tadhmini ya michuano hiyo. Anasema hakika mashindano hayo yamepoteza uelekeo kutokana na klabu kuleta wachezaji ambao wamezidi umri ambao unatakiwa.
Ukweli ni kwamba michuano hayo imepoteza uhalisia wake, klabu zimekiuka taratibu na kuleta wachezaji ambao wamepita umri ambao unatakiwa. Nafikiri kufanya hivyo si kuikomoi TFF bali tunaiweka timu yetu ya Taifa kwenye mazingira magumu,
Naye kocha wa Small Kids ya Rukwa, John Willium Del Piero alisema mashindano hayo yameonyesha mafanikio makubwa kutengeneza wachezaji isipokuwa anashauri kuendeshwa sawa na Ligi Kuu.
Timu 15 kucheza ligi kwa majuma mawili ni sawa na bonanza, nafikiri haitoi fursa nzuri kwa vijana hao kuonyesha vipaji vyao,
Nafikiri TFF wakitafuta wadhamini zaidi kwa mashindano haya, ni wazi mambo yatakuwa mazuri, kwani ushindani utaongezeka.

Friday, November 25, 2011

Lady Jay Dee-TEJA

REBECCA BLACK-FRIDAY

Neema-DDC Mlimani Park

SIMBA Vs AZAM HAPATOSHI FAINALI YA VIJANA LEO KARUME

TIMU za Simba na Azam FC zote za jijini Dar es Salaam, leo zinakutana katika mechi ya fainali inayotarajia kubeba taswira kubwa ya ushindani ya michuno ya Kombe la Vijana chini ya umri wa miaka 20 kwenye Uwanja wa Karume.
Upinzani wa mechi hiyo uko wazi kutokana na ubora ulioonyeshwa na vikosi hivyo mpaka kufikia hatua ya kucheza fainali.
Michuano hiyo maalum kwa ajili ya kukuza vipaji, ilianza wiki mbili zilizopita na kupigwa kwenye viwanja vya Karume na Chamazi kilichopo nje kidogo ya jiji.
Simba ilikata tiketi ya kucheza fainali hizo baada ya kuifunga Toto African kwa mabao 4-1 katika mechi ya nusu fainali. Ushindi huo wa Simba ulikuwa kama kulipa kisasi kwani katika mechi ya kwanza baina ya timu hizo Toto waliifunga Simba bao 1-0.
Kwa upande wa Azam walitinga hatua ya fainali baada ya kuifundisha soka timu ya taifa ya vijana (U-17), Serengeti Boys kwa kuiangushia kipigo cha mabao 3-0.
Timu za Toto African na Serengeti Boys, zitatangulia kushuka dimbani kucheza mechi ya kusaka mshindi wa tatu, ambapo mshindi ataondoka na shilingi 500,000 na medali za Fedha.
Bingwa wa mashindano hayo ya kila mwaka, atajinyakulia shilingi 1.5milioni, Kombe na medali za Dhahabu, huku mshindi wa pili akipata medali za Shaba na kitita cha shilingi 1milioni.
Mbali na hizo pia, kutakuwa na zawadi za Mchezaji Bora atajipatia shilingi 400,000. Mfungaji Bora shilingi300,000, Kipa Bora shilingi 300,000, na timu yenye nidhamu itapata shilingi 300,000.
Makocha wa pande zote mbili Simba na Azam wametamba kila mmoja kwa upande wake kutwaa kombe hilo kulingana na kikosi chake kilivyojiandaa.
Vijana wangu wako kwenye hali nzuri ya pambano hilo na wamenihakikishia kucheza kufa na kupona kutwaa kombe hilo," alisema Seleman Matola kocha wa Simba kama ilivyo kocha wa Azam Iddy Cheche.
Msimu uliopita Ruvu Shooting ndiyo iliyotwaa kombe baada ya kuwafunga 'ndugu' zao JKT Ruvu kwa mabao 2-1 katika mechi ya fainali. Msimu huu mabingwa hao hawakuweza kufua dafu.