Thursday, June 16, 2011

BAMBO APATA AJALI YA PIKIPIKI AVUNJIKA MGUU.

Wasanii wakimuangalia Bambo kitandani kwa huzuni.

Dereva wa pikipiki iliyokodiwa na Bambo akiwa hoi hospitalini.

Msanii maarufu wa maigizo Dickson Makwaya a.k.a BAMBO leo alfajiri maeneo ya Kigogo amepata ajali mbaya ya pikipiki, baada ya pikipiki aliyokuwa ameikodisha kugongwa na daladala aina ya DCM na kusababisha Bambo kuvunjika mguu wa kulia sehemu ya paja huku ajali hiyo ikimuacha dereva wa pikipiki hiyo akiwa katika hali mbaya, wote wamelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu. 

No comments:

Post a Comment