Tuesday, June 7, 2011

WAJUE 10 WANAOWANIWA NA ARSENE WENGER.

Meneja wa timu ya Arsenal ya uingereza Arsene Wenger amnahusishwa na nia ya kuhitaji wachezaji ambao atawatumia kujenga kikosi cha timu ya Arsenal ambacho kimemaliza ligi na hali mbaya japokuwa kilikuwa kikiwania ubingwa kwa karibu zaidi, wachezaji ambao wapo kichwani mwa Wenger ni hawa wafuatao. 
1-Gervinho, mshambuliaji wa Lille ya ufaransa raia wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 24 ambaye anauzwa kwa dau la paundi za uingereza milioni 12-15.


2-Borjan Kric,Mshambuliaji wa Barcelona na raia wa uhispania mwenye umri wa miaka 20 dau lake ni paundi za uingereza milioni 16-18. 

3-Mamadou Sakho,mlinzi wa kati wa PSG na raia wa ufaransa mwenye umri wa miaka 21 dau lake ni paundi za uingereza milioni 12-18.

4-Jan Vertonghen,Mlinzi wa kati wa Ajax na raia wa ubelgiji, umri miaka 24,dau lake ni paundi za uingereza milioni 12-15.
5-Gary Cahill, Mlinzi wa kati wa Bolton na raia wa uingereza, umri miaka 25,dau lake ni paundi za uingereza milioni 15-20.

6-Phil Jones, Mlinzi wa kati wa Blackburn na raia wa uingereza, umri miaka 19, dau lake ni paundi za uingereza milioni 15-18.

7-Karim Benzema, Mshambuliaji wa Real Madrid na raia wa Ufaransa,umri miaka 23, dau lake ni paundi za uingereza milioni 20-26.

8-Christopher Samba, Mlinzi wa kati wa Blackburn na raia wa Congo, umri miaka 27, dau lake ni paundi za uingereza Milioni 8-12.

9-Radamel Falcao,Mshambuliaji wa Porto na raia wa Colombia, umri miaka 25, dau lake ni paundi za uingereza milioni 26.


10-Ricardo Alvarez, mshambuliaji wa pembeni wa Velez Sasfield na raia wa Argentina, umri miaka 23, dau lake paundi za uingereza milioni 6-12.

ARSENE WENGER
wakati huo huo wenger anatafuta mrithi wa Niclas Bendtner mbali na hao kumi katika kumrithi Bendtner wengine ni Jeremy Menez wa Roma ya italy, Hugo Rodallega waWigan Athletic,Hulk wa Porto F.C, Gonzalo Higuian wa Real Madrid na Eden Hazard wa Lille.

No comments:

Post a Comment