Tuesday, July 26, 2011

ASTON VILLA YAKUBALI KUTOA DAU KUMNYAKA N'ZOGBIA TOKA WIGAN

Charles N'zogbia
Aston Villa imefungua milango ya maongezi na Wigan Athletic juu ya kumsajili Charles N'zogbia mwenye umri wa miaka 25 na imekubali kulipa ada ya uhamisho ya paundi za uingereza 9.5 milioni. Meneja wa Villa Alex Mc Leish ameridhishwa na kiwango cha N'zogbia na timu yake imeamua kufanya mazungumzo rasmi na Wigan ili kumsajili mchezaji huyo. Habari kutoka ndani ya klabu ya Villa zinasema pesa ipo ya usajili baada ya kumuuza Ashley Young kwenda Man United na Stewart Downing kwenda Liverpool zote za uingereza, kabla ya kusaini mkataba mrefu ndani ya Villa N'zogbia anatarajiwa kwanza kufanyiwa vipimo vya afya.

No comments:

Post a Comment