Tuesday, July 26, 2011

MANCINI ANA MATUMAINI YA KUMNASA SERGIO AGUERO

Meneja wa Man City Roberto Mancini amefunguka na kusema kuwa ana matumaini makubwa ya kumnasa Sergio Aguero kutoka Atletico Madrid mwishoni mwa wiki hii. Man C inafungua milango ya maongezi na Atletico Madrid kwa kuwa Srgio amekuwa ni mmoja kati ya wachezaji anaowahitaji katika kikosi chake.
Sergio Aguero
Pamoja na upinzani uliopo kutoka kwa Real Madrid na Juventus ambao nao wanatajwa kumuwania Sergio lakini Mancini ana matumaini ya kushinda kinyang'anyiro hicho mwishoni mwa mwezi huu."Sielewi kwa sasa lakini ninachojua Atletico walikuwa na maongezi na Sergio kabla ya mwisho wa wiki" alisema Mancini.
"Nafikiri kati ya siku nne au tano kabla ya mechi inayofuata,na inaweza kuwa wiki hii tukamaliza mazungumzo"Alioneza Mancini.
"Aguero amecheza Copa America, kama tukikubalina nataka nizungumze nae mwenyewe kwasababu nataka nijue maoni yake(kuhusu kucheza Manchester City)" Alifunguka zaidi kocha huyo wa Manchester City.

No comments:

Post a Comment