Friday, August 5, 2011

CHELSEA YASAJILI MBRAZIL WA BARCELONA

Chelsea imemsajili mchezaji wa kiungo Oriol Romeu kwa mktaba wa miaka minne kutoka klabu ya Barcelona kwa kitita cha paundi milioni 4.35.

Oriol Romeu
Ada hiyo ya uhamisho iliafikiwa siku 11 zilizopita.
Romeu atawasili Stamford Bridge mara atakapomaliza kuichezea timu ya taifa ya Hispania iliyo katika mashindano ya Kombe la Dunia chini ya umri wa miaka 20 nchini Colombia.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 ameshacheza mechi zote hadi sasa katika mashindano hayo ikiwemo waliyoshinda mabao 4-1 dhidi ya Costa Rica na walipoilaza Ecuador 2-0.
Romeu msimu uliopita alicheza mara mbili katika kikosi cha kwanza cha Barca, akicheza mechi yake ya kwanza kwa timu ya wakubwa mwishoni mwa msimu uliopita, lakini hakuwemo katika kikosi cha muda mrefu cha kocha Pep Guardiola.
Kiungo huyo ambaye alikuwa zaidi akicheza katika kikosi cha pili cha Barcelona, alisema wiki hii: "Chelsea ni chaguo muhimu kwangu.
Kusajiliwa kwa Romeu ni faraja kubwa kwa bosi mpya wa Chelsea Andre Villas-Boas ambaye kwa muda wa miezi sita ijayo atamkosa kiungo muhimu Michael Essien.
Essien aliumia goti wakati wa mazoezi ya kujiandaa na msimu.


No comments:

Post a Comment