Friday, August 26, 2011

Fainali UEFA Super Cup ni BARCELONA vs F.C PORTO leo

 FC Barcelona vs FC Porto
Leonel Messi mchezaji bora wa ulaya 2011-2012

Fainali ya UEFA super Cup Leo inawakutanisha wababe wawili yaani Barcelona ya Spain na F.C Porto. Mchezo huo utakaopigwa leo 26 agosti 2011 majira ya saa 18:45-20:45 GMT katika dimba la Stade Louis II jijini Monaco.
Barcelona bingwa mtetezi wa kombe hilo anakutana na bingwa wa ligi ya ulaya F.C Porto, Barcelona imeshachukua kombe hilo mara 3 wakati F.C Porto wamelinyaka mara 1 tu, Barcelona ni ya 2 kwa ubora ulaya 2011-2012 na F.C Porto ni ya 7 kwa takwimu za Shirikisho la soka la ulaya(UEFA).

Katika mechi hiyo timu zinatarajiwa kupangwa kama ifuatavyo;

FC Barcelona :
David Villa, Lionel Messi, Victor Valdes, Adriano Correia, Daniel Alves; Sergio Busquets, Xavi Hernandez, Andres Iniesta, Eric Abidal, Javier Mascherano, Pedro Rodriguez.


FC Porto :
Helton,Fucile, Souza, Joao Mourinho, Freddy Guarin, Alvaro Pereira, Rolando, Otamendi, Varela/James Rodriguez, Kleber, Hulk.

No comments:

Post a Comment