Monday, October 24, 2011

SIMBA YANGA ZAWABANGUA MAAFANDE KUKUTANA USO KWA MACHO JUMAMOSI 29 Oktoba 2011

SIMBA, juzi walizidi kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu Bara baada ya kuilaza Ruvu Shooting mabao 2-0, katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 24 na kuzidi kukalia kiti cha ligi hiyo, huku ikiwa imecheza mechi 10 na kuiacha JKT Oljoro ikiwa ya pili kwa kujikusanyia pointi 19.

Ruvu Shooting walikuwa wa kwanza kulifikia lango la Simba, dakika ya sita, Abdallah Juma, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyoipata kwa kupiga mpira nje ya lango.

Dakika tano baadaye, Kassim Linde, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyopata baada ya kupiga shuti lililotoka nje.

Simba walijibu mashambulizi, dakika ya 16, Emmanuel Okwi, alipiga shuti kali lililookolewa na mabeki wa Ruvu Shooting.

Mshambuliaji Uhuru Seleman, dakika ya 25, alipiga shuti kali lililogongwa mwamba wa goli na kuokolewa na mabeki Shooting.

Hassan Dilunga wa Ruvu Shooting, alipata nafasi nzuri ya kufunga dakika ya 42, lakini mpira aliopiga ulitNa Speciroza Joseph

SIMBA, jana walizidi kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu Bara baada ya kuilaza Ruvu Shooting mabao 2-0, katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 24 na kuzidi kukalia kiti cha ligi hiyo, huku ikiwa imecheza mechi 10 na kuiacha JKT Oljoro ikiwa ya pili kwa kujikusanyia pointi 19.

Ruvu Shooting walikuwa wa kwanza kulifikia lango la Simba, dakika ya sita, Abdallah Juma, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyoipata kwa kupiga mpira nje ya lango.

Dakika tano baadaye, Kassim Linde, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyopata baada ya kupiga shuti lililotoka nje.

Simba walijibu mashambulizi, dakika ya 16, Emmanuel Okwi, alipiga shuti kali lililookolewa na mabeki wa Ruvu Shooting.

Mshambuliaji Uhuru Seleman, dakika ya 25, alipiga shuti kali lililogongwa mwamba wa goli na kuokolewa na mabeki Shooting.

Hassan Dilunga wa Ruvu Shooting, alipata nafasi nzuri ya kufunga dakika ya 42, lakini mpira aliopiga ulitoka nje ya lango.

Simba, ambao walipata nafasi sita za mpira wa adhabu, lakini walishindwa kuzitumia nafasi hizo.

Dakika ya 47, Okwi, aliwainua mashabiki wa Simba, baada ya kuifungia timu yake bao akitumia vizuri mpira ulioanza kwa Haruna Moshi 'Boban' aliyempasia Jerry Santo, kabla ya mfungaji wa bao hilo kuukwamisha wavuni.

Boban aliyeingia kuchukua nafasi ya Uhuru Seleman, aliifungia bao la pili Simba, dakika ya 54, kwa shuti la mbali lililomshinda kudaki kipa wa Ruvu Shooting, Benjamin Haule.

Bao hilo linakuwa na pili kwa wachezaji wazawa, baada ya Kapombe kufunga katika mechi dhidi ya African Lyon wiki iliyopita. Mabao 12 ya Simba, yamefungwa na wachezaji kutoka nje ya nchi.

Kufungwa kwa bao hilo, kuliwazindua Shooting ambao walikuwa wakisaka mabao ya kusawazisha, hata hivyo walikutana na ngome imara iliyokuwa ikiongozwa na Juma Nyosso na Obadia Mungusa.

Simba: Juma Kaseja, Nassoro Masoud 'Cholo', Juma Jabu, Juma Nyosso, Obadia Mungusa, Patrick Mafisango/Shomari Kapombe, Jerry Santo, Ulimboka Mwakingwe, Emmanuel Okwi, Felix Sunzu, Uhuru Seleman/Haruna Moshi 'Boban'.

Ruvu Shooting: Benjamin Haule, Michael Pius, Paul Ngalema, George Michael, Shaban Suzan, Iddi Nyambiso, Ayoub Kitala, Hassan Dilunga, Abdallah Juma/Seif Abdallah, Kassim Linde/ Juma Mdindi, Raphael Keyala/Abdallah Abdulrahman.
oka nje ya lango.

Simba, ambao walipata nafasi sita za mpira wa adhabu, lakini walishindwa kuzitumia nafasi hizo.

Dakika ya 47, Okwi, aliwainua mashabiki wa Simba, baada ya kuifungia timu yake bao akitumia vizuri mpira ulioanza kwa Haruna Moshi 'Boban' aliyempasia Jerry Santo, kabla ya mfungaji wa bao hilo kuukwamisha wavuni.

Boban aliyeingia kuchukua nafasi ya Uhuru Seleman, aliifungia bao la pili Simba, dakika ya 54, kwa shuti la mbali lililomshinda kudaki kipa wa Ruvu Shooting, Benjamin Haule.

Bao hilo linakuwa na pili kwa wachezaji wazawa, baada ya Kapombe kufunga katika mechi dhidi ya African Lyon wiki iliyopita. Mabao 12 ya Simba, yamefungwa na wachezaji kutoka nje ya nchi.

Kufungwa kwa bao hilo, kuliwazindua Shooting ambao walikuwa wakisaka mabao ya kusawazisha, hata hivyo walikutana na ngome imara iliyokuwa ikiongozwa na Juma Nyosso na Obadia Mungusa.

Simba: Juma Kaseja, Nassoro Masoud 'Cholo', Juma Jabu, Juma Nyosso, Obadia Mungusa, Patrick Mafisango/Shomari Kapombe, Jerry Santo, Ulimboka Mwakingwe, Emmanuel Okwi, Felix Sunzu, Uhuru Seleman/Haruna Moshi 'Boban'.

Ruvu Shooting: Benjamin Haule, Michael Pius, Paul Ngalema, George Michael, Shaban Suzan, Iddi Nyambiso, Ayoub Kitala, Hassan Dilunga, Abdallah Juma/Seif Abdallah, Kassim Linde/ Juma Mdindi, Raphael Keyala/Abdallah Abdulrahman.


YANGA YAISAMBARATISHA JKT OLJORO
Wakati huohuo jana Yanga ya Dar es salaam wameiadhibu Timu ya maafande wa JKT Oljoro kwa bao 1-0 katika uwanja wa Chamanzi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Kazi nzuri ya mshambuliaji wa kimataifa Haruna Nyonzima akiwatoka akiwazidi ujanja mabeki wa Oljoro na kutoa pande maridadi kabisa lililomkuta Hamis Kiiza akiwa katika nafasi nzuri ya kushinda nae bila ajizi akaachia kombora kali lilioenda mojo kwa moja kimiani na kuihakikishia timu yake ya Yanga ushindi wa goli 1-0 katika mechi hiyo.

No comments:

Post a Comment