Monday, November 14, 2011

Bunge Sports kushiriki mashindano ya mabunge ya Afrika mashariki Bujumbura

TIMU ya soka ya Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeingia kambini mjini Dodoma kujiandaa na michuano ya wabunge wa mabunge ya Afrika Mashariki, michuano itakayofanyika, Bujumbura, Burundi kuanzia Novemba 20.

Kocha wa timu hiyo, Kassim Majaliwa alisema kuwa kikosi chake kitaondoka Dodoma Novemba 19 kikiwa na wachezaji 25.Aliwataja wachezaji watakaoandamana na timu hiyo kuwa ni Amos Makala, William Ngeleja, Kighoma Malima, Sadifa Juma, Masauni Masauni, Erasto Zambi, Juma Nkamia na Steven Ngonyani.

Wachezaji wengine wanaounda timu hiyo ni; Haeshi Khalfan, Muiguru Mchemba, Ali Kingwangwala, Abdul Mteketa, Ngwali Juma, Victor Kawawa, Fakhi Haji Fakhi, Mahamoud Mgimwa, Chris Kimnyonyele na Job Lusinde.

Majaliwa ambaye ni Naibu Waziri wa Tamisemi aliwataja wengine kuwa ni Mambi Mumbala, Mark Kilumbi, Kassim Fundi na Michael Kadebe wakati daktari ni Kassim Ramadhani na Cesilia Sanya.

Mashindano hayo yatashirikisha nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Tanzania na wenyeji Burundi. Mwaka jana yalifanyika Arusha na Tanzania ilitwaa ubingwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Prof. Maji Marefu alisema maandalizi yanakwenda vizuri na timu yake iko vizuri kutetea ubingwa.

No comments:

Post a Comment