Monday, November 14, 2011

Esperance yatwaa ubingwa wa Afrika



BEKI Harrison Afful aliifungia bao la ushindi, Esperance ya Tunisia katika mechi ya fainali ambayo Wydad Casablanca waliokuw 10 uwanjani walilala kwa bao 1-0 katika mchezo wa pili wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Afful alifumania nyavu katika dakika ya 21, aliingia ndani ya eneo la hatari na kuachia mkwaju uliopmpita kipa wa Wydad, Yassine Bouno—aliyesimama langoni kuchukua nafasi ya mkongwe Nadir Lamyaghri aliyeumia mazoezini.

Esperance iliyotwaa ubingwa mara ya mwisho 1994, wakati Wamorocco wa Wydad walitwaa ubingwa mwaka ’92.Timu hizop mbili kutoka Kaskazini mwa Afrika zilitoka suluhu katika mchezo wa kwanza uliofanyika kwenye mji wa Casablanca wiki moja iliyopita.

Wydad ilipunguzwa kasi baada ya mchezaji wake, Mourad Lemsen kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Yannick N’Djeng.Esperance iliyopigwa 6-1 na TP Mazembe ya DR Congo katika fainali ya mwaka jana. Esperance pia iliingia fainali mwaka 1999 na kufungwa na Raja Casablanca Morocco kwa penalti na mwaka uliofuata ilifungwa na Hearts of Oak.

Lakini safari hii ikicheza mbele ya mashabiki 50,000 waliojazana Stade 7 November mjini Rades walikuwa na kila sababu ya kushinda.Baada ya bao, Afful alitengeneza mipira mingi ikiwemo wa dakika ya 28 alipomtolea pande Oussama Darragi, akiwa ndani ya eneo la hatari, alipaisha mpira huo.

Wydad ilishindwa kusawazisha nafasi ya wazi katika dakika ya 32 wakati Fabrice Ondama lakini shuti lake liliokolewa na kipa wa Esperance, Moez Ben Cherifa.

No comments:

Post a Comment