Friday, November 11, 2011

Reggie Love"Obama's little Brother" kuacha kazi na kuondoka Ikulu ya Marekani "WHITE HOUSE"


Obama na Reggie wakicheza mpira wa kikapu.

Huenda hakuna msaidizi wa ikulu ya Marekani aliye karibu zaidi na Rais Obama zaidi ya Reggie Love, Love mwenye umri wa miaka 30 ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu na kikapu ambaye amekuwa msaidizi wa Rais Obama tangu kipindi alipokuwa seneta.

Akiwa msaidizi binafsi wa Obama Love amekuwa nae karibu zaidi bila hata kuacha umbali wa futi kadhaa pindi anaposaini Aotographs na anapoweka "swaga" kwa ajili ya kupiga picha.

Amekuwa karibu zaidi na Obama na mara nyingi wamekuwa wakicheza Mpira pamoja na Obama amekaririwa akisema Reggie Love ni mdogo wake na mtu wake wa karibu ambavyo hajawahi kutokea,na sasa anaondoka.



Muda wa mazoezi..Obama akiwa katika jogging,Reggie hayuko mbali

Reggie akiwaonesha jambo maafisa wa Ikulu pamoja na Rais Obama


Nipe Gwala...Obama akimpa tano Reggie

Obama ndani ya Gari na "mdogo wake" Reggie



Obama akiteta jambo na Reggie

Obama akifunga kwa staili ya Lay up

Obama na Reggie wakikatiza mitaa kuelekea mazoezini

Reggie kipindi anacheza mpira wa Kikapu na timu ya Duke

Love akipiga chabo kwanza kabla ya Obama kutoka


Obama na Reggie ndani ya ndege ya rais




Ikulu ya Marekani haijatoa taarifa zaidi ya kuondoka kwa Reggie Love lakini watu wa karibu wamesema Reggie anataka ajikite zaidi katika kumalizia Masters yake katika chuo kikuu cha Pennsylvania (University of Pennsylvania's Wharton Business School).

No comments:

Post a Comment