Monday, January 30, 2012

Arsenal yailipua Aston Villa kombe la F.A

Robin Van Persie na Theo Walcott
Van Persie na Walcott

Robin van Persie ilibidia afanye kazi ya ziada Jumapili, na hatimaye akifunga magoli mawili ya penalti, na kuiwezesha Arsenal kuponea chupuchupu kuondolewa katika raundi ya nne ya Kombe la FA, baada ya kupambana na Aston Villa, hatimaye ikishinda 3-2.
Kufikia mwisho wa nusu ya kwanza ya mchezo, Arsenal ikichezea uwanja wa nyumbani wa Imarati, tayari ilikuwa imeachwa nyuma kwa magoli 2-0.
Arsenal vs Aston Villa

Mabao hayo yalikuwa yamefungwa na Richard Dunne (kwa kichwa) na goli la mkwaju wa kupinda kupitia mchezaji Darren Bent.
Lakini magoli matatu katika muda wa dakika saba yaliubadilisha mchezo kabisa, na Van Persie akibadilisha mambo kwa mkwaju wa penalti, baada ya Dunne kumchezea vibaya Aaron Ramsey.
Theo Walcott alisawazisha kabla ya Van Persie kuandikisha ushindi, kwa kupata bao la pili la penalti, kufuatia Bent kucheza mchezo usio halali dhidi ya Laurent Koscielny.
Arsenal, mabingwa mara 10 wa Kombe la FA, sasa watacheza na mshindi atakayepatikana katika mchezo wa raundi ya nne utakaorudiwa kati ya Middlesbrough na Sunderland.
Sunderland na Middlesbrough walipocheza katika mechi ya awali Jumapili mchezo ulikwisha kwa sare ya 1-1.
The Gunners watacheza mechi hiyo wakifahamu sasa wana uwezo wa hatimaye kuendelea na mashindano hayo, na kuwaletea mashabiki wao kombe ambalo wamelisubiri kwa muda mrefu.
Katika droo ya raundi ya tano, ambayo imefanyika Jumapili, klabu ya daraja ya kwanza, Stevenage, kwa mara ya kwanza katika historia yake imekuwa miongoni mwa timu 16 zilizosalia katika mashindano hayo, na sasa itacheza na Tottenham.
Brighton itasafiri hadi uwanja wa Anfield kucheza na Liverpool, Chelsea nao ni wenyeji wa Birmingham, na Crawley Town, katika daraja ya pili, itacheza na Stoke.
Sunderland ikifuzu baada ya mechi ya marudiano, itapambana na Arsenal.
Norwich itacheza na Leicester, na Everton itaikaribisha Blackpool.
Bolton itacheza aidha na Millwall, au Southampton.

No comments:

Post a Comment