Wednesday, January 25, 2012

Breaking NEWS: Washiriki BIG BROTHER AFRICA 7 Kushiriki na wapenzi wao



Unaweza kupata nafasi ya kushiriki katika shindano la Big Brother Afrika 7 mwaka huu kuanzia februari 5 lakini lakini hautashiriki peke yako utahitajika kuingia na mpenzi wako.

Waandaji wa Big Brother Afrika wameleta mshangao "suprise" nyingine katika mashindano hayo baada ya kutangaza kuwa katika mashindano ya mwaka huu washiriki wote kila mmoja atahitajika kuingia mjengoni na mpenzi wake.
Katika hali ya kushangaza zaidi mshindi wa mwaka huu atajinyakulia kitita cha dola za kimarekani 300,000 na ili kunyakua kitita hiki utaingia katika shindano ukiwa na mpenzi wako.

Kwahiyo kama utaamua kuingia na baba,mama,dada,kaka,rafiki wa kike,rafiki wa kiume,mpenzi,mchumba,mume,mke au yeyote lakini ili mradi muwe wawili (pair), je,nani atayatoa maisha pamoja na wewe? kumbuka unaweza kutumia muda mwingi na mtu ulieingia nae kama mpenzi wako hivyo kuwa makini katika kuchagua nani wa kuingia nae.

Katika shindano la mwaka huu waandaaji wametangaza Ethiopia kushiriki kwa mara ya kwanza katika mashindano hayo. Ina maana ili ushiriki mwaka huu lazima uwe na mwenzi wako kutoka katika nchi wasiriki kama ifuatavyo Angola, Botswana, Ghana, Kenya, Liberia, Malawi, Namibia, Nigeria, Sierra Leone, South Africa, Tanzania, Uganda, Zambia and Zimbabwe.
Wapenzi lazima wawe wametoka nchi moja, wawe wanajua kuzungumza vizuri lugha ya kiingereza,umri miaka 21 na kuendelea  na wawe na pasi ya kusafiria iliyo hai (valid passport).

Fomu za kushiriki zitanza kutolewa tarehe 5 februari na mwisho itakuwa tarehe 27 februari. kwenye mtandao fomu zitapatikana kwenye mtandao wa www.endemol.co.za .
Kazi kwenu mnaotaka kuuza sura na mademu zenu ndani ya nyumba wahini mkajiandikishe mimi mwenzenu tayari.

No comments:

Post a Comment