Monday, January 30, 2012

Djokovic bingwa Australia open amchabanga Nadal, Azarenka bingwa kwa wanawake

Novak Djokovic
Djokovic bingwa wa Tennis kwa wanaume

Novak Djokovic kutoka Serbia, Jumapili alimshinda Rafael Nadal kutoka Uhispania, katika fainalil ya mashindano ya tennis ya Australian Open, iliyofanyika mjini Melbourne.
Djokovic alipata ushindi wa 5-7, 6-4, 2-6, 6-7, 7-5.
DJOKOVIC VS NADAL

Pambano hilo sasa limeandikishwa katika historia kama shindano ambalo limechukua muda mrefu zaidi katika historia ya mashindano ya tennis ya Open.
Ushindi huo wa tatu mfululizo katika mashindano ya Grand Slam, umemchukua Djokovic muda wa saa tano, na dakika 53.
Limeandikisha historia pia kwa kuwa pambano la muda mrefu zaidi kwa mchezaji mmoja kwa mmoja katika mashindano ya Australian Open.
Akimpongeza mpinzani wake, Djokovic alimsifu Rafael Nadal, akisema ni kati ya wachezaji bora zaidi katika historia ya tennis.
Alimpongeza pia kwa pamoja wote kuandikisha historia ya fainali ya muda mrefu zaidi, na akitumaini kwamba watakutana katika mapambano mengine siku zijazo, ila Jumapili ilikuwa haiwezekani kuwapata washindi wawili kwa pamoja.
Fainali ya kitambo ya Grand Slam iliyochukua muda mrefu zaidi ilikuwa ni mwaka 1988, mashindano ya US Open, wakati Mats Wilander, raia wa Sweden, alipomshinda Ivan Lendl, mchezaji wa Czechoslovakia, na ambaye baadaye alibadilisha uraia na kuwa Mmarekani.
Pambano hilo lilichukua muda wa saa 4, dakika 54.

Azarenka

Azarenka vs Sharapova

Kwa upande wa fainali ya kina dada, siku ya Jumamosi, Victoria Azarenka alimshinda Maria Sharapova na kupata ushindi wake wa kwanza wa mashindano ya Grand Slam.
Ushindi huo umemfanya kuwa ni nambari moja sasa katika tennis ya kina dada ulimwenguni.
Azarenka, mwenye umri wa miaka 22, na ambaye ni raia wa Belarus, alimshinda Sharapova kutoka Urusi 6-3 6-0, baada ya muda wa saa nzima, na dakika 22.

No comments:

Post a Comment