Monday, January 30, 2012

Ghana yailiza Mali

Andre Dede Ayew
Ayew akishangilia goli la pli la Ghana

Ghana inaelekea kufuzu kwa robo fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya Jumamosi kuishinda Mali magoli 2-0.
Asamoah Gyan ndiye aliyefunga bao la kwanza la Black Stars.
Ghana vs Mali

Andre 'Dede' Ayew kisha aliwachanganya walinzi wa Mali na kupitia nafasi iliyojitokeza, aliandikisha bao la pili la Ghana.
Awali Cheick Diabate mara mbili ilikuwa nusra aifungie Mali magoli, lakini kweli bahati haikuwa yake, kwani mipira yote iligonga goli, lakini kamwe mpira ulikataa kugusa nyavu katika mechi hiyo iliyochezewa mjini Franceville.
Ghana inaongoza kundi D kwa pointi sita, lakini kimahesabu, mataifa ya Guinea na Mali bado yana nafasi ya kufuzu kuingia robo fainali.
Guinea kwa hakika ilithibitisha uwezo wake katika mashindano hayo kwa kuiangamiza bila huruma Botswana, magoli 6-1, katika mechi ambayo pia ilichezewa mjini Franceville.
Guinea inatazamia wingi huo wa mabao huenda ikawa jambo zuri, na inasubiri kwa hamu kusikia matokeo ya mechi kati ya Mali na Botswana Jumatano ijayo mambo yatakuwa vipi, na wakati ambao wao watacheza na Ghana.

No comments:

Post a Comment