Wednesday, February 15, 2012

Arsenal AC Milan kivumbi ligi ya mabingwa ulaya


Kocha wa Arsenal Arsene Wenger

AC Milan watakuwa na lengo moja la kuifunga timu ya England kwa mara ya kwanza tangu walipofanya hivyo dhidi ya Liverpool kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka 2007, wakati watakapowakaribisha Arsenal katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ya mashindano hayo.
Milan iliyotwaa taji hilo mara saba kwa kuifunga Liverpool 2-1 jijini Athens miaka mitano iliyopita, baada ya hapo wamekuwa wakitolewa kwenye mashindano hayo na Arsenal, Manchester United na Tottenham Hotspur na alifanikiwa kupata sare dhidi ya Portsmouth kwenye hatua ya makundi ya Europa Ligi mwaka 2009.
Sasa wanakutana na Arsene Wenger kwa mara nyingine baada ya timu hiyo ya London kuwatoa Milan kwenye hatua ya 16 bora mwaka 2008.
Vinara hao wa Serie A, Milan watamtumia mshambuliaji wake Zlatan Ibrahimovic aliyefungiwa kucheza ligi kwa kumpiga kibao mchezaji baada ya kumaliza kifungo Jumamosi waliposhinda 2-1 dhidi ya wapinzani wao mbio za ubingwa wa Italia, Udinese huku chipukizi Stephan El Shaarawy na Maxi Lopez wakionyesha uwezo mkubwa wa kufunga.
Chipukizi El Shaarawy huenda akawekwa benchi ili kumpisha Ibrahimovic pamoja na kuwa kwenye kiwango cha juu kwa sasa na inavyoonekana kama mshambuliaji wa Sweden wataanza pamoja na Robinho.
Kocha Massimiliano Allegri ana wachezaji wengi majeruhi, lakini kumeonekana na mabadiliko kidogo na kutoa nafasi ya kurejea kwa kipa Christian Abbiati na beki wa kati Alessandro Nesta kuivaa Arsenal, ambayo imeshinda mechi zake zote za Ligi ya Mabingwa ilizocheza San Siro dhidi ya Milan.
Gennaro Gattuso na Alberto Aquilani bado ni majeruhi, lakini kuna nafasi ya Alexandre Pato na Kevin-Prince Boateng kuwepo kikosi leo.
Mabingwa watetezi Milan wanaongoza Serie A kwa tofauti ya pointi mbili, lakini Juventus inayoshika nafasi ya pili ina mchezo moja mkono.
“Ushindi wetu dhidi ya Udinese una maana kubwa, tumetoka kufungwa mechi tatu kati ya tano,” alisema kocha Allegri.
Milan, iliyofuzu kwa hatua hiyo pamoja na mabingwa watetezi Barcelona, hadi sasa wameshindwa kurudia mafanikio yao ya mwaka 2007.

MBINU za WENGER

Mafanikio katika mchezo huo ni mbinu atakayotumia Wenger kama atacheze kwa kujilinda zaidi na kutaka sare au kujaribu kushambulia ili kupata ushindi wake wa tatu dhidi ya Milan.

Wenger anatakiwa kujihadhari pia na mashambulizi ya Milan kwa kucheza kwa uangalifu zaidi, lakini kiungo wake Aaron Ramsey anaamini bao la ugenini linaweza kuwa jibu la mafanikio yao.Aliimbia Arsenal TV Online: “Kama tutacheza na kufanikiwa kupata bao na kurudi Emirates hayo yatakuwa matokeo ya kujivunia zaidi kwetu.
“Ni matumaini yangu, tutaweza kupata mabao mengi ya kuweza kuwaondoa kwenye mashindano.”
Vikosi:

AC Milan: 32-Christian Abbiati; 20-Ignazio Abate, 33-Thiago Silva, 5-Philippe Mexes, 15-Djamel Mesbah; 23-Massimo Ambrosini, 4-Mark Van Bommel, 10-Clarence Seedorf; 27-Kevin-Prince Boateng; 11-Zlatan Ibrahimovic, 70-Robinho
Arsenal: 13-Wojciech Szczesny; 3-Bacary Sagna, 5-Thomas Vermaelen, 6-Lauren Koscielny 17-Alex Song; 8-Mikel Arteta, 7-Tomas Rosicky, 16-Aaron Ramsey, 15-Alex Oxlade-Chamberlain; 10-Robin van Persie, 14-Theo Walcott

Mwamuzi: Viktor Kassai (Hungary).

No comments:

Post a Comment