Friday, February 10, 2012

BIG UP TIMBULO WANAOSEMA NA WASEME


Timbulo

BIG UP TIMBULO,..Wale wote wanaosema Timbulo kakopi ule wimbo wa Domo langu kutoka kundi la Xmalea wa Ivory Coast nawapinga vikali, Timbulo amekiri aliipata hiyo ngoma kabla na akachukua idea tu na sio kukopi kama inavyosemwa mitaani.
Kwa kifupi nampongeza sana Timbulo hata kama idea ni ya mtu lakini ametumia ujuzi mwingi katika kutunga na kuimba mpaka song likatoka poa..wanaomsema na nyinyi jaribuni kukopi halafu mtoe song likubalike kama mnaona ni rahisi.

Song la Timbulo Domo langu

Nimesikiliza kipindi mtoto Adam Mchomvu anamponda Timbulo kwa kusema eti kakopi na kupesti, nadhani elimu Adam hana ya nini maana ya kukopi na kupesti. Kukopi na kupesti inamaana haubadilishi kitu unachukua kitu kama kilivyo toka sehemu moja na kukiweka sehemu nyingine bila kupunguza ama kuongeza kitu.
Katika song waliloimba hao wa Ivory Coast wameimba lugha tofauti na melody tofauti, Hapo utaona kazi kubwa ameifanya Timbulo ya kupata idea halafu akatafuta mashairi yake binafsi yakaendana na ile idea halafu akaimba kwa ustadi mpaka ikakubalika sio kazi ndogo kama unabisha jaribu wewe uone kama utapata kitu.
Ni kazi sana kuchukua idea ya mtu halafu ukatoa kitu kikakubalika kuliko kile kilichokupatia idea kuliko kutoa kitu chako binafsi, mara nyingi hata wasanii wa nje huwa wanajitahidi kutoa track kali na inapofikia kutoa remix wanahakikisha iwe kali kuliko track halisi, haina maana ukitoa track kali ikapendwa halafu ukatoa remix ikawa utumbo inakuwa haina maana.
Mwisho kabisa Adam na wenzako naomba niwape maana ya sanaa na msanii inawezekana hamjui ndio maana mnaropoka tu.

Sanaa ni upangaji wa dhana kulingana na hisia na mawazo ya msanii, na msanii ni mtu anaepanga dhana kulingana na hisia na mawazo yake.
Timbulo songa mbele wanaopiga kelele ni mashabiki wa muziki na sio wapenzi wa muziki kwani kuna tofauti kubwa kati ya mshabiki na mpenzi.
Big up Timbulo kama kukopi ni rahisi hakuna asietaka track yake iwe juu waambie na wao wakopi tuone.

No comments:

Post a Comment