Friday, February 10, 2012

PINDA anastahili kuwajibishwa


Waziri mkuu Mizengo Pinda

Madaktari wamerudi makazini baada ya kuafikiana na serikali kutoka katika mgomo uliodumu kwa takribani wiki mbili.
Sasa basi kama serikali ina uwezo wa kuwasikiliza madaktari na wakaafikiana warudi makazini kama alivyofanya waziri mkuu Mh Mizengo Kayanza Pinda, kwanini hawakuwasikiliza mapema na wakaafikiana kabla ya watanzania wasio na hatia kupoteza maisha yao kutokana na mgomo huo?
Ina maanisha serikali imefanya uzembe kwa kitu ambacho wana uwezo nacho,na uzembe huo umesababisha usumbufu,maumivu,gharama,hasara na VIFO vya watanzania walipa kodi walioiweka serikali hii madarakani, je ni nani anawajibika katika hili? nani atafidia gharama,muda,maumivu na VIFO vya watanzania wasio na hatia kutokana na mgomo huo wa madaktari uliodumu kwa takribani wiki mbili?
Kwa ukweli huu je? nitakuwa nina makosa kama nikisema Viongozi wote wenye dhamana katika serikali hii wawajibike kwa hili, nina maanisha kuanzia Rais wa nchi na "mnyororo" wote unaofuatia baada ya yeye.

Watanzania wenzangu nina uchungu mkubwa kutokana na vifo vya watu wasio na hatia kupoteza maisha kwa uzembe wa watu wachache tena ambao wapo kwa ridhaa ya wananchi walioteseka na waliopoteza maisha kutokana na uzembe wa serikali wa kutokuwasikiliza wananchi wanahitaji nini kwa wakati gani. Ni nani serikalini alikuwa hajui kuwa madaktari wanaandaa mgomo? bila shaka madaktari ni watu wasomi na makini sidhani kama walikurupuka tu asubuhi na kusema leo tunagoma bila sababu na bila taarifa, kama matatizo na sababu zao kugoma zilijulikana kwanini wakapuuzwa na wao kufikia hatua ya kugoma na kusababisha hasara,maumivu na VIFO vya watanzania walipa kodi wasio na hatia? wapo wanapaswa kuwajibika kuanzia kiongozi aliepokea taarifa hizo kama alitakiwa kuzifikisha kwa anaefuatia baada ya yeye na anaefuatia mpaka mwenye maamuzi ya mwisho wote hawa wanapaswa kuwajibika.

Naipinga kauli ya Waziri mkuu Mizengo Pinda alipotangaza kuwa serikali imeamua kuwasimamisha kazi naibu katibu mkuu Wizara ya afya na ustawi wa jamii mama Blandina Nyoni na mganga mkuu wa serikali Dk Deo Mtasiwa, na kusema kuwa swala la mawaziri kuwajibika ni la kisiasa. Hapa mkuu sijakuelewa kabisa swala la huduma na haki ya jamii wewe unasema ni la kisiasa? BIG NO, wanapaswa kuwajibika haraka sana.

Watanzania wenzangu hatutaonekana wakorofi au hatufai kama tukiishinikiza serikali kuwawajibisha wote waliopo katika utekelezaji wa madai ya madaktari kwa kuwa hakuna lolote linaloweza kulipa machungu ya wafiwa na maisha ya watanzania waliopoteza maisha pasipo hatia
MUNGU IBARIKI TANZANIA     MUNGU WABARIKI WATANZANIA HASA WALALAHOI

No comments:

Post a Comment