Tuesday, February 7, 2012

Mechi ya Yanga kuhamishiwa Sudan ni sawa na kuruka maji na kukanyaga matope


Wapiganaji wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan

Sehemu ya uwanja ikiungua baada ya kutokea vurugu kati ya mechi ya Al-ahly dhidi ya Al-masry nchini Misri

Mechi ya Yanga na Zamalek kuhamishiwa Sudan kutoka Misri kutokana na vurugu zilizotokea Misri na kuua mashabiki uwanjani, Uamuzi huo ni sawa na kuruka maji na kukanyaga matope.
Kama timu zinahofia kucheza Misri kutokana na kuhofia usalama wao sidhani kama Sudan ni sehemu salama, kwani hivi sasa Sudan kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe na mgogoro mkuu ukiwa ni mafuta yanayopatikana katika mipaka ya Sudan kusini na Khartoum,huku serikali mbili zikishutumiana kila moja ikimhofia mwenzake kuwasaidia waasi wanaosababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Hata hivyo, Sudan inaweza kuwa si sehemu salama sana kwani mwaka 2009 wakati wa mechi ya mwisho ya kufuzu kwa Kombe la Dunia 2010 iliyozikutanisha Misri na Algeria kulitokea vurugu na mamia ya mashabiki kujeruhi.

No comments:

Post a Comment