Tuesday, April 10, 2012

ARSENAL YAICHAKACHUA MAN CITY, MAN U YAUA


Muuaji wa Man City Mikel Arteta Kulia

Mkwaju wa mbali wa Mikel Arteta umeipa Arsenal ushindi muhimu na kuiacha Manchester City ikiwa pointi nane nyuma ya Manchester United katika ligi kuu ya England.
Yaya Toure alitoka mapema kutokana na kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na David Pizzaro huku Balotelli akitolewa kwa kadi nyekundu.
Mara mbili Robin Van Persie aligonga mwamba huku mkwaju mwingine aliopachika wavuni ukiwa wa kuotea.
Arteta alipata mwanya katika dakika ya 86 kwa kuachia mkwaju umbali wa yadi 25.
Arsenal sasa wamerejea katika nafasi ya tatu, pointi mbili juu ya Tottenham walio nafasi ya nne.
Schioles
PAUL SCHOLES

Shuti kali la Scholes lilihakikisha ushindi wa United
Awali manchester United iliichapa QPR kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Old Trafford.
Man United sasa imefikisha pointi 79, City ikifuatia na pointi 71 ikiwa imesalia michezo sita kumalizika kwa ligi.

No comments:

Post a Comment