Thursday, April 19, 2012

NAHODHA WA UINGEREZA APIGWA MIMBA, KUIKOSA OLIMPIKI


Nahodha wa timu ya soka ya wanawake ya Uingereza Faye White

Kukiwa kumesalia siku mia moja kwa michezo ya Olimpiki kuanza kutimua barafu mjini London ,Kapteni wa timu ya Soka ya Uingereza ya wanawake Bi Faye White atayakosa mashindano hayo.
Bi White hataichezea timu yake ya taifa Uingereza wakati wa Olimpiki kwa sababu ana mimba.
Bibi huyo mwenye umri wa miaka 34 ambaye nyumbani anachezea timu ya soka ya wanawake ya Arsenal amesema anatarajia kujifungua mwezi wa Oktoba.

Faye awapo uwanjani shughuli yake si ndogo hata kidogo

Bi White amedokeza kuwa huenda pia akajiuzulu kutoka timu hiyo ya taifa mara tu baada ya kujifungua
" Nina mimba na kwa mara ya kwanza kufikia mwezi wa Oktoba nitakuwa mama” aliiambia BBC.
Kapteni huyu atakumbukwa kwamba wakati wa robo fainali ya kombe la dunia kwa akina dada mwaka wa 2011 walipochuana na Ufaransa alikosa mkwaju wa penaliti.
Bi White anasema hana uhakika kama baada ya kujifungua ataendelea kuchezea klabu yake ya Arsenal au atastaafu kabisa kutoka mchezo huo.

Bi Faye akiwa kwenye uzi wa chama lake la Arsenal

No comments:

Post a Comment