Wednesday, May 9, 2012

LIVERPOOL YALIPA KISASI KWA CHELSEA YAIBAMIZA 4-1


Caroll akibinjuka tik-tak mbele ya beki wa Liverpool

Ikiwa ni siku tatu tu baada ya Chelsea kuichapa Liverpool katika fainali ya kombe la FA kwa
Ivanovic aliesimama na Essien alielala wakishuhudia mpira uliopigwa na Suarez na kumgonga Essien ukitumbukia kimiani

magoli 2-1. Hatimaye Liverpool wakiwa katika dimba lao la Nyumbani pale Anfield wamewararua Chelsea kwa kamba 4-1 bila huruma mbele ya mashabiki 40,721 waliohudhuria mtifuano huo.


Luis Suarez akishangilia goli la kwanza la Liverpool

Kiama cha Chelsea kilianza katika dakika ya 18 pale Suarez alipoilamba vyenga ngome ya Chelsea na kuingia na mpira mpaka kwenye eneo la hatari pembeni ya uwanja alipoingiza kati mpira kwa ufundi na ukamgonga Essien na kutumbukia kambani na kuandika bao la kuongoza kwa Liverpool.

Caroll na Henderson wakishangilia kamba ya pili iliyotupiwa na J Henderson

Iliwachukua dakika 24 Liverpool kuendeleza kipigo pale J Henderson alipotupia kambani goli la pili kwa Liverpool na kuwaacha Chelsea wakiwa hawaamini kimbunga kinachowanyemelea.

Mara nyingine tena D Agger katika dakika ya 27 alitupia kambani bao la tatu ambalo kwa kiasi kikubwa liliwanyong'onyesha Chelsea kama sio kuwazorotesha na mbwembwe zote za Ubingwa wa FA zikawatokea puani.

J Hernandes waoooooooooooooooooooo

Mungu sio Athumani mnamo dakika ya 49 mchezaji mwenye juhudi na bidii na ubishi wa kiafrika ingawa ni mbrazili Ramires aliipatia Chelsea bao la kupangusia machozi ya kipigo katika mechi hiyo.


Mtifuano kati ya Terry na Suarez

Wakati kila mtu akiamini kichapo kimefikia mwisho, Golikipa wa akiba wa Chelsea alifanya boko la maana pale alipiga mpira katikati ya uwanja ili hali hayupo golini na ndipo kingekewa cha kupata goli kilipomuangukia J Shevley nae bila ajizi akatupia kambani kwa shuti kali katika dakika ya 60 na kuhitimisha dhoruba kali la mabao 4-1 kwa Chelsea toka kwa Liverpool.
Poleni sana fans wa Chelsea msife moyo mnaweza jipoza kwa Bayern Munich haa haaa haaaaaaa!!!

No comments:

Post a Comment