Monday, August 27, 2012

WAZIRI WA USALAMA LIBYA AJIUZULU


Waziri wa usalama wa Libya aliejiuzulu Fawzi Abdel A'al

Taarifa kutoka Libya zinasema kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Fawzi Abdel A'al, amejiuzulu.
Sababu ya kujiuzulu kwake haijafahamika mara moja.

Kujiuzulu kwa bwana Fawzi kumetokea siku moja baada ya polisi katika mji mkuu, Tripoli, kutuhumiwa kushindwa kuwazuwia Waislamu wenye msimamo mkali wasibomoe msikiti na kaburi la Wasufi mchana kweupee.

No comments:

Post a Comment