Monday, September 10, 2012

OBAMA ABEBWA JUU JUU NA MUUZA PIZZA


Rais Obama akiwa amenyanyuliwa juu na Scott Van Duzer

Mmiliki wa Mgahawa maarufu jijini Florida, Marekani Scott Van Duzer alitoa kali ya mwaka alipotembelewa na Rais Obama katika mgahawa wake na kumnyanyua juu kama ishara ya furaha aliyikuwa nayo kwa ujio wa Obama pale mgahawani.

Rais Obama akitumia usafiri wa basi katika ziara ya siku mbili jijini Florida ikiwa ni sehemu za kampeni za uchaguzi utakaofanyika mwezi Novemba, alitembelea Mgahawa maarufu jijini Florida unaotambulika vilivyo kwa kuuza Pizza baaab kubwa unaojulikana kama Big Apple Pizza & Pasta Restaurant unaomilikiwa na Scott Van Duzer.

"Scott, what's going on, man," alisikika rais Obama akisalimiana na Van Duzer mara tu ya kuingia mgahawani. "Let me tell you, you are like the biggest pizza shop owner I've ever seen."  Obama aliendelea kumwaagia misifa Van Duzer ambae alimpigia kura rais Obama mwaka 2008 na ameahidi kumpigia tena kura mwezi Novemba.


Woooowww jamani rahaaa sio rahaaaa...Van Duzer akimkumbatia President Obama na kumnyanyua juu juu katika mgahawa anaoumiliki wa Big Apple Pizza & Pasta Restaurant jijini Florida,Marekani.

No comments:

Post a Comment