Monday, November 26, 2012

MAN CITY, CHELSEA HAKUNA MBABE

Timu za soka za Chelsea na Man City ziliumana katika mwendelezo wa mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza katika uwanja wa Stamford Bridge.
Katika mpambano huo wa wababe hao kutoka suluhu na ikiwa mechi ya kwanza kwa kocha mpya wa Chelsea Rafael Benitez akichukua nafasi ya kocha kipenzi cha mashabiki wa Chelsea Roberto De Matteo.
Mashabiki wa Chelsea hawakufurahishwa na kitendo cha De Matteo kutimuliwa na wameonesha kwa kiasi kikubwa hawamkubali kabisa Rafael Benitez ambaye ameshindwa kuipa matumaini mema Liverpool alipokuwa kocha mkuu na sasa yupo Chelsea itakuwaje? ngoja tusubirie lakini mashabiki na mimi mwenyewe hatumkubali Benitez kama tunavyomkubali De Matteo.




Mashabiki wa Chelsea na ujumbe wa kumdhihaki Benitez na kumtukuza De Matteo


Benitez akiwa kibaruani lakini mashabiki hawamkubali hata kidogo

Roberto Mancini kocha wa Man City akitoa maelekezo katika mpambano huo


Huu Haaa!! Kazi Vicent Company na Torres


Tulia wewe bwana mdogo tuu!!! Torres akiwa chini ya ulinzi mkali


Ukijipendekeza nakupasua!!! Ramires akimtuliza Aguero


Aaaah mi nimeshachoka msiniseme sana bhanaa wanakaba kama nini!!

No comments:

Post a Comment