Monday, November 26, 2012

MPIGIE KURA MCHEZAJI UNAYETAKA ACHUKUE TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA 2012 YA BBC

Majina ya wachezaji watano wanaowania tuzo la BBC la mchezaji bora zaidi barani Afrika mwaka 2012 yamewekwa hadharani.

Bofya Yahya Toure.
Mcheza kiungo kutoka Ivory Coast, anayeichezea Manchester City ya Uingereza. Toure aliiongoza Manchestert City kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 44 iliyopita.


Bofya Demba Ba
kwa sasa ni mmoja wa wachezaji nyota wa klabu ya Newcastle na kufikia sasa tayari amefunga jumla ya magoli 6 katika ligi kuu ya premier la England na anatarajiwa kujumuishwa kwenye kikosi cha Senegal kitakachocheza katika fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika.


Bofya Didier Drogba
Ni noadha wa timu ya taifa ya Ivory Coast, amewahi kuongoza Chelsea kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England pamoja na kombe la klabu bingwa barani ulaya.


Bofya Christopher Katongo
Ni mchezaji wa timu ya taifa ya Zambia maarufu kama Chipolopolo na aliiongoza timu hiyo kushinda fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika


Bofya Younes Belhanda
Ni mchezaji mwenye umri wa miaka 22, na mmoja wa wachezaji waliotia fora na kuisaidia klabu ya Montepellier, kushinda kombe la ligi kuu kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya karne moja tangu klabu hiyo ilipobuniwa.

PIGA KURA HAPA
Bofya Ukitaka kupiga kura unaweza kufungua anwami hii ya mtandao na kumbuka maagiza yametolewa kwa lugha ya Kiingereza.

No comments:

Post a Comment