Wednesday, December 19, 2012

MESSI BADO YUPO SANA BARCELONA

Lionel Messi amekubali kusaini mkataba mpya na klabu ya Barcelona, utakaodumu kwa mwaka wa 2018.

Nyota huyo kutoka Argentina, mwenye umri wa miaka 25, amekuwa na miaka minne ya mafanikio na klabu hiyo na pia kwa taifa lake.

Kufikia sasa Messi amefunga jumla ya magoli 90 mwaka huu pekee.

Mlinda langu Carles Puyol, 34, na mcheza kiungo Xavi Hernandez, 32, pia wamesaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Barcelona.

Ripoti zinasema kuwa wachezaji hao sasa watasalia na Barcelona hadi mwaka wa 2016.

Kwa mujibu wa tangazo kutoka kwa klabu hiyo, Puyol, Messi na Xavi wanatarajiwa kusaini mkataba mpya katika muda wa siku chache zijazo.

Afisa mmoja wa klabu hiyo amesema ni jambo la kutia moyo kuona kuwa Barcelona imefanikiwa kudumisha huduma za wachezaji wake nyota.

Kandarasi ya Messi na Barcelona inakamila mwa wa 2016 ili hali kandarasi ya Puyol inamalizika mwaka wa 2013 huku kandarasi ya Xavi inakamilika mwaka wa 2014.


Leonel Messi

No comments:

Post a Comment