Tuesday, December 11, 2012

TAIFA QUEENS BINGWA WA MABARA WAICHAKAZA MALAYSIA KATIKA FAINALI

wachezaji wa timu ya taifa ya Netiboli, wakiwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere, wakitokea Singapore walikokuwa wakishiriki mashindano ya mabara na kuibuka mabingwa. Hakika wanastahili pongezi
Taifa Queens ilipowasili nchini

Timu ya netiboli ya Tanzania (TAIFA QUEENS) imeibuka kidedea na kushinda mchezo wa fainali dhidi ya Malaysia kwa kuibanjua mabao 45-38. Kwa matokeo hayo Taifa Queens imetawazwa kuwa bingwa wa mabara kwa mwaka huu wa 2012 (IFNA Inter-Continental netball title). 
Mashindano hayo yaliyofanyika Nchini Singapore  ambayo bingwa mtetezi alikuwa Australia yameshuhudia Taifa Queens ikimaliza mashindano bila kupoteza mchezo hata mmoja. Mwenyekiti wa Chaneta Anna Bayi amesema mpaka timu zinaenda mapumziko tayari Taifa Queens walikuwa mbele kwa mabao 25-16, Waliporudi kipindi cha pili ilikuwa kumalizia kazi nzuri waliyoianza.

Timu hiyo imewasili nchini jana na kombe la mabara na medali za dhahabu na kuleta heshima mpya kwa Tanzania katika anga ya michezo, Ikumbukwe Taifa Queens ilitembeza bakuli balaa mpaka kufikia kuelekea Singapore huku wadau wenye kuweza kudhamini michezo wameng'ng'ania kupanda mbegu zisizoota kwenye mpira wa miguu, Wakati umefika wadau kuigeukia michezo mingine na huenda mungu akatujaalia kama jinsi nyota inavyoanza kuonekana katika sekta ya michezo nchini.

Hongereni sana Taifa Queens kwani mmetutoa kimasomaso na sasa Tanzania itaanza kutamkwa bila kung'atang'ata maneno katika anga za michezo duniani.

Taifa Queens wakifanya vitu vyao..wacha weeee..kalieni soka tu halafu tuone tutafika wapi!!

Weyee, Chezea Taifa Queens weweeee!!!

Sisi ndio sisi bhanaaaaa mtausaka kwa tochi hamuupati ngodo!

No comments:

Post a Comment