Monday, January 21, 2013

ARSENAL YAZAMA DARAJANI

Chelsea imeweza kupata pointi tatu muhimu katika kinyang'anyiro cha ligi kuu ya Soka England baada ya kuipasua Arsenal magoli 2-1 katika uwanja wa Stanford Bridge.

Juan Mata alitupia bao la kwanza la Chelsea kabla ya Frank Lampard kuhitimisha machungu ya mashabiki wa Arsenal kwa kufunga bao la pili kupitia mkwaju wa penalti.

Hata hivyo Arsenal kupitia kwa mshambuliaji wake Theo Walcott aliweza kufunga bao zuri, akiwazidi maarifa walinzi wa Chelsea pamoja na mlinda mlango mahiri Peter Cech.

Kipindi cha Arsenal ilizidi kuibana Chelsea ambapo ilipata kona tisa dhidi ya tatu za Chelsea. Hata hivyo mechi hiyo ilimalizika kwa Chelsea kuibuka na ushindi huo wa magoli mawili kwa moja.

Huu ni ushindi wa kwanza kwa Chelsea katika uwanja wake mwaka huu 2013 kati ya mechi nne ilizocheza uwanjani hapo Stanford Bridge.

Wachezaji wa Chelsea wakishangilia goli la kwanza

Torres akijaribu kuwatoka mabeki wa Arsenal

Lampard akipiga penati kuandika bao la pili

Walcott akitupia kambani goli la Arsenal

Walcott akishangilia goli na mchezaji mwenzake Jack Wilshere
Chelsea 2-1 Arsenal

No comments:

Post a Comment