Ilikuwa katika dakika ya 7 tu ya mchezo pale Yaya Toure alipotupia kambani goli la kwanza kabla ya Jonathan Ayite kusawazisha katika dakika ya 45 sekunde chache kabla ya mapumziko. Timu zote zilirudi uwanjani na nguvu mpya kila moja ikitafuta ushindi lakini katika mchezo huo uliotawaliwa zaidi na nyota wa Ivory Coast na dakika 3 kabla mchezo kumalizika mshambuliaji "mchoyo" wa Arsenal Gervinho aliweza kuipatia Ivory Coast goli la pili na la ushindi. Mpaka mwisho Ivory Coast 2-1 Togo.

Yaya Toure akishangilia goli na wachezaji wenzake

Adebayor chini ya ulinzi mkali

Togo wakishangilia goli la kusawazisha


Drogba akionesha udambwidambwi..
Gervinho wa Ivory Coast akitiririka na gozi la ng'ombe

Gervinho akishangilia goli
Ivory coast 2-1 Togo
No comments:
Post a Comment