Friday, May 25, 2012

NCHUNGA AACHIA KITI KUINUSURU YANGA..Chezea wazeiya weye!!!


Mwenyekiti wa Yanga alieachia ngazi Lloyd Nchunga

Vicky Kimaro(Gazeti la Mwananchi)SIKU moja baada ya kuvamiwa nyumbani kwake usiku wa manane na kundi la watu wasiojulikana Mwenyekiti wa Yanga, Lloyd Nchunga amejiuzulu kuiongoza klabu hiyo.

Nchunga alitangaza uamuzi huo wa kujiuzulu jana jijini Dar es Salaam kwenye ofisi yake iliyopo jengo la NSSF Akiba mbele ya waandishi wa habari wachache.

Alisema,"sipo tayari kuona klabu Yanga inahujumiwa kwa vile tu mimi ni kiongozi, Kamati ya Utendaji na wale walioteuliwa chini ya ibara ya 29(3) ya katiba ya Yanga pamoja na bodi ya wadhamini, itawaongoza wanachama mpaka kufikia mkutano mkuu kwa mafaniko zaidi."

"Kwa hekima nimeamua kujiuzulu nafasi yangu katika Uenyekiti wa Yanga kwani ni klabu ninayoipenda hata kama mimi sio kiongozi kwa mujibu wa ibara ya 28 ya katiba yetu,"alisema Nchunga.

Katika siku za hivi karibuni Nchunga amejikuta kwenye mgogoro mkubwa na Baraza la Wazee la klabu hiyo ambao walikuwa wakimshinikiza ajiuzulu kwa madai kuwa ameisababisha madeni makubwa klabu hiyo ikiwa ni pamoja na mwenendo mbovu wa timu yao huku wakidai wachezaji wamekosa nidhamu.

Pia wazee hao walikuwa wakimlaumu Nchunga kwa kusababisha Yanga kupata matokeo mabovu katika mchezo dhidi ya watani zao wa jadi Simba walipofungwa mabao 5-0 katika mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu ya Tanzania bara.

Nchunga akizungumza jana na waandishi wa habari alisema kitendo kinachofanywa na Baraza hilo la Wazee wakiongozwa na Ibrahimu Akilimali ni usaliti mkubwa ulioambatana na matukio mbalimbali yanayoendelea ndani ya klabu hiyo hadi kuupindua uongozi wake.

"Siwatuhumu wachezaji moja kwa moja, isipokuwa mfululizo wa matukio wiki tatu kabla ya mchezo na Simba inaonyesha kulikuwa na usaliti mkubwa ambao hatukuweza kuubaini mapema,"alisema Nchunga.

"Sioni mantiki kwa hoja kuwa tulifungwa kwa vile wachezaji walikuwa wakidai mishahara, posho, au eti mtendaji wetu alishikiliwa Arusha kwa deni la hoteli, ndiyo tuvune bao tano,"alisema Nchunga.

Alisema,"kwa wanaoijua Yanga wanafahamu Yanga imewahi kuwa na madeni makubwa katika hoteli mbalimbali, mawakala wa ndege na baadhi tumeyakuta sisi na kuyalipa, hii imewahi kutokea kabla na wakati akiwapo mfadhili, sembuse sisi tulioachwa baki na bado wachezaji walicheza kwa morali?."

"Uongozi wangu ndani ya mwaka mmoja tumechukua mataji matatu, ubingwa wa Ligi Kuu, 2011/2012, Kombe la Kagame na Ngao ya Hisani ukiachia mechi ya Mei 6 ambayo tulifungwa magoli matano,"alisema Nchunga.

Alisema,"tumefanikiwa kuboresha mkataba wetu na TBL, tumeingia mkataba na Nexus Ltd ambao inatutafutia wadhamini wa ndani na nje, tumefanya kampeni kupitia mitandao na kukusanya data za wanachama na kusajili wapya lengo likiwa ni kukusanya Sh3,000,000 hadi 8,000,000 kwa mwaka kwa kipindi cha miaka mitatu."

Nchunga alisema,"hayo yote tulifanya ili kuondokana na utegemezi wa ufadhili wa mtu mmoja na tayari tulishatuma maombi kwa msajili Manispaa ya Ilala ya kuanzisha Saccoss ya Yanga."

"Utamaduni wa kutimuana baada ya matokeo mabaya ni dhambi ambayo itatutafuna kama hatutaiacha, kwani wenye hila na uchu wa madaraka wataendelea kutumia mbinu hiyo ili kuondoa uongozi wa kidemokrasia,"alisema Nchunga akiwa na sura ya huzuni.

Alisema,"baada ya Mapinduzi kushindikana na TFF kuonya, wazee wakiongozwa na Akilimali wamesikika katika kipindi cha michezo cha radio moja wakidai ni bora Yanga ishushwe daraja au kufungiwa kuliko mimi kuendelea kuongoza.

Katika hatua nyingine Nchunga pia, alisema jana majira ya saa nane usiku alisikia mbwa wakibweka kwa nguvu huku taa za alamu zikipiga kelele mfululizo kitendo ambacho kilimstua na alipochungulia dirishani aliona kundi la watu wanaokadiriwa kufikia 15 wakiwa kwenye harakati za kutaka kuingia ndani kwake.

"Baada ya kusikia kelele zile za alamu na mbwa tuliwapigia simu walinzi wetu wawili kumbe na wenyewe walikuwa wameshafanya jitihada za kutafuta nguvu kwa walinzi wengine kitendo kile kililiogopesha kundi lile na kukimbilia bondeni, hata hivyo tulipiga simu polisi ambao walifika na kukuta kundi hilo limeshatoweka,"alisema Nchunga.

Alisema,"suala hilo hivi sasa lipo Polisi na upelelezi unaendelea ili kubaini waliohusika katika kitendo kile."

CHADEMA IKO JUU, CHEZEA MNYIKA WEWE!


John Mnyika,Mbunge wa Ubungo(CHADEMA) aliyeshinda kesi ya uchaguzi.

Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la Ubungo umeunguruma katika mahakama kuu kanda ya Dar es salaam na mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika (Chadema) amemshinda tena Hawa Ng'humbi (CCM) baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kutoa hukumu kuwa ushindi wa Mbunge Mnyika uliofanyika Oktoba 31, 2010 ulikuwa wa halali.

Kesi hiyo namba 107 ya 2010, ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ngh’umbi dhidi ya Mnyika ambaye ni mdaiwa wa pili katika kesi hiyo akitetewa na Wakili Edson Mbogoro.

Mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo iliyoko mbele ya Jaji Upendo Msuya ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi (RO) katika jimbo hilo, (aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni) ambao walikuwa wakitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali (PSA), Justice Mulokozi.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika Oktoba 31, 2010, Msimamizi wa Uchaguzi, Raphael Ndunguru alimtangaza Mnyika kuwa mshindi Novemba 2, 2010 baada ya kupata kura 66,742. Ngh’umbi alipata kura 50,544.

Hata hivyo, Ngh'umbi hakuridhishwa na matokeo hayo akaamua kufungua kesi Mahakama Kuu kuyapinga, akimtumia Wakili Issa Maige.

Katika hati yake ya madai na wakati akitoa ushahidi mahakamani, Ngh’umbi na mashahidi wake walidai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu na kisheria katika ujumlishaji wa kura na utangazaji wa matokeo ambao umeathiri matokeo hayo.

Tuesday, May 22, 2012

HAPA NDIPO AMBAPO HAMNA MAANA YA KUVAA (KOFIA)HELMET







HII NDIO MARCEDES MAYBACH YENYE THAMANI YA DOLA MILIONI 1.3


Marcedes Maybach Inavyoonekana kwa mbele


Sehemu ya ndani mbele


Sehemu ya ndani nyuma ambapo unaweza kujiachia kama jamaa anavyopata udambwidambwi


Pale kati ina sehemu ya kuhifadhia glasi na vinywaji vya kila aina ili mradi umatemate uwe unaruhusu tu


Unaweza kujiachia namna hii na kusahau kama kuna siku utaiaga dunia na starehe hizo ukawaaachia wenzio


ACHA NDOTO SASA RUDI KATIKA MAISHA YA UWEZO WAKO ALAAAAAH

Huu ndio saizi yetu..au mnasemaje?

BOBAN AANGUUKA NA KUZIMIA UWANJA WA NDEGE


Mgosi na Boban wakiwa katika msiba mjini Kinshasa

MICHAEL MOMBURI, KINSHASA
KIUNGO wa Simba, Haruna Moshi Boban, ameanguka katika Uwanja wa Ndege wa N`Djili mjini Kinshasa kutokana na mapigo ya moyo kushuka ghafla.

Tukio hilo lilitokea jana Jumatatu wakati Boban akiwa anajiandaa kurudi Dar es Salaam baada ya kuhudhuria mazishi ya Patrick Mafisango aliyefariki Alhamisi iliyopita kwa ajali ya gari iliyotokea jijini Dar es Salaam.

Hali ya Boban ilibadilika ghafla akiwa uwanjani hapo na akashindwa kuona mbele kabla ya kulegea na kuanguka.

Madaktari wa uwanja huo walitumia zaidi ya saa 1:30 kumtibu Boban kabla hajarejea katika hali ya kawaida huku bado akiwa na simanzi kubwa kutokana na kifo cha Mafisango.

"Nilimkumbuka sana Mafisango, wakati nikitafakari, nikaona ninalegea, nikashindwa kuona kitu chochote mbele na nikaanguka," Boban aliliambia Mwanaspoti katika uwanja huo wa ndege wa Kinshasa.

Daktari aliyemuhudumia Boban aliliambia Mwanaspoti kuwa: "Alikuwa na hali mbaya sana, mapigo ya moyo yalikuwa chini, yangeweza kuondoa maisha yake."

Licha ya kupata matibabu hayo, Boban pia alipewa kahawa kwa lengo la kuinua mapigo yake ya moyo.

Boban ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Mafisango ikiwa ni pamoja na kulala chumba kimoja wanapokuwa kambini Simba, aliwakilisha wachezaji wengine wa klabu hiyo katika msiba huo mjini Kinshasa.

Mwili wa Mafisango aliyekuwa akicheza nafasi ya kiungo enzi za uhai wake, ulizikwa katika makaburi ya Kinkole nje kidogo ya Kinshasa juzi Jumapili kuhitimisha safari yake ya miaka 32 ya uhai wake duniani.

MILOVAN ALAMBA DUME SIMBA SPORTS CLUB


Kocha Milovan(Kushoto) na mwenyekiti wa Simba(Kulia)Rage

Timu ya Simba Sport Club ambao ni mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara wamemuongezea mkataba kocha wao Milovan Cirkovic kwa miaka miwili zaidi na kumfanya kocha huyo kuwa na uhakika na "umatemate" zaidibaada ya ule waliokuwa wamempa mwanzo wa miezi sita kumalizika.
Mkataba uliomalizika wa Milovan ni baada ya kurithi mikoba ya Mganda Moses Basena, akitangaza kumuongezea mkataba huo kocha Milovan, Makamu mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange Kaburu amesema" Kipimo cha mafanikio ya kocha ni mataji na soka safi,kitu ambacho sisi kama viongozi wa Simba tumekishuhudia chini ya Profesa Milovan,sasa hatuoni kwanini tusimuongezee mkataba."
Kaburu aliongeza kuwa sababu nyingine ni mipango mizuri aliyonayo Milovan kwa soka la Vijana wa Simba, ni kitu ambacho hakipingiki katika ligi iliyokwisha tumeshuhudia Vijana wa Simba wakipata nafasi ya kucheza na dhahiri wameonesha uwezo wao,mfano mzuri Jonas Mkude,Singano na wengine yote hayo ni mafanikio ya kocha Milovan kuwapa nafasi Vijana kuonesha "udambwidambwi" wao.

NADAL BINGWA ITALIAN OPEN AMCHAPA DJOKOVIC


Rafael Nadal (Kushoto) akiwa amebeba kombe la Ubingwa wa Italian Open baada ya kumshinda Djokovic(Kulia)

Rafael Nadal, mchezaji wa Uhispania, alifanikiwa kumshinda mchezaji bora zaidi duniani wa kiume, Novak Djokovic katika mashindano ya Italia Open, na kupata ubingwa wake wa sita katika mashindano hayo ya Italia.

Nadal alipata ushindi wa 7-5 6-3 katika fainali hiyo ambayo ilichezwa Jumatatu baada ya kuahirishwa siku ya Jumapili kutokana na mvua kunyesha mno mjini Roma.

Ushindi huo umemweka Nadal katika nafasi ya pili katika orodha ya wachezaji bora zaidi katika mashindano ya wanaume duniani.


Pamoja na hali ya hewa kuwa si shwari lakini wapenzi wa mchezo wa Tennis waliendelea kufuatilia mtifuano huo kati ya Nadal an Djokovic

Kabla ya mashindano ya Jumatatu, Djokovic, raia wa Serbia, amekuwa akimshinda Nadal mfululizo katika mashindano saba yaliyopita, kabla ya kuanza kuibuka tena kama mshindi katika fainali ya Monte Carlo Masters mwezi uliopita.
Sasa Nadal amemshinda katika fainali mbili za mwisho walizokutana.

Nadal alisema: "Mawazo ya ushindi yalinijia wakati muwafaka, kwani kumshinda Novak, unahitaji kuwa katika hali yako bora zaidi ya uchezaji, kwani yeye hukusukuma hadi mjwisho katika pambano lote.

"Nadhani kiakili nilikuwa katika hali thabiti kila wakati muhimu nilipohitajika kuwa hivyo."
Nadal Vs Djokovic