Thursday, August 23, 2012

LEO NDIO LEO BARCELONA Vs REAL MADRID



Kocha wa Barca Tito Vilanova

Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho

TITO Vilanova alikuwa Barcelona kama msaidizi wa Pep Guardiola wakati alipotawala vichwa vya habari Agosti mwaka jana baada ya kuchapwa kibao cha usoni na kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho kwenye mchezo wa Hispania Super Cup.

Leo ni mwaka umepita tangu tukio hilo limetokea na Tito amechukua jukumu la rafiki yake la kuifundisha Barca sasa anakutana tena na Mourihno katika mchezo wake wa kwanza mgumu kama kocha utakaofanyika kwenye Uwanja wa Nou Camp (saa 5:30 usiku).

Mabingwa watetezi Barca wamefuzu kucheza hatua hiyo baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Mfalme na hiyo itakuwa mechi ya kwanza ya kupima ubora wa kikosi cha Vilanova dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu.

Uhasama baina ya wachezaji uliosabishwa na kadi tatu nyekundu kwa wachezaji wa Real mwaka 2011 pamoja na picha za televisheni kuonyesha Mourinho akimzaba kibao Vilanova umepungua kwa kiasi kikubwa.

Tukio hilo lilisababisha Mourinho kufungiwa mechi mbili za Super Cup, na Vilanova mechi moja kwa kuonyesha ishara mbaya, lakini adhabu hizo zote zimefutwa na rais wa shirikisho la soka la Hispania, Angel Maria Villar.

Mourinho, amekataa kuomba msamaha kwa yeyote, lakini mashabiki wa Madrid wamejitokeza na kukiriki kuwa kocha wao alifanya kosa.

Imeanza Ligi Vyema,
Barca imeanza vizuri kampeni zake za kusaka ubingwa wa ligi kuu kwa ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Real Sociedad Jumapili iliyopita, huku wapinzani wake Real Madrid wakilazimishwa sare 1-1 nyumbani na Valencia.

Kuanza vizuri kwa Vilanova katika ligi kumechagizwa na kurejea kwa mshambuliaji wake David Villa aliyekuwa nje kwa zaidi ya miezi nane baada ya kuvunjika mguu, lakini Jumapili alifanikiwa kufunga bao kwenye ushindi wao mnono wa mabao matano.

Mshambuliaji huyo wa Hispania bado hajawa fiti na kuna uwezekano leo akapumzishwa kama itakavyokuwa kwa kiungo mpya Alex Song.

Mchezaji pekee mwenye uhakika wa kuanza leo ni Lionel Messi ambaye msimu uliopita alifunga mabao 73 ndiye atakayeongoza mashambulizi dhidi ya Real.

"Timu bado imebaki ile ile na falsafa na mtindo ni ule kama ilivyokuwa enzi za Guardiola," Messi aliimbia Barca TV.

"Bado wachezaji wote wanahamu ya kupata mataji. Nataka kushinda kila kitu na kocha Tito."

Kinara wa ufungaji wa Real, Cristiano Ronaldo bado hajawa fiti na katika mchezo wa kwanza wa ligi uliofanyika kwenye uwanja wa Bernabeu alishindwa kupiga hata shuti moja golini.

"Bado sijawa fiti kwa asilimia 100, lakini natumaini nitarudi kwenye kiwango changu haraka," alisema Ronaldo.

Mreno mwenzake Pepe ameondolewa kwenye kikosi kitachocheza mechi hiyo baada ya kuumizwa wakati alipogongana na kipa wake Iker Casillas kwenye mchezo wao wa Jumapili dhidi ya Valencia.

Pamoja na Barca kutawala sana mechi za 'clasicos' chini ya Guardiola, lakini Real wamepoteza mechi moja tu wakiwa na Mourinho kati ya mara nne walizokutana Catalunya

Wednesday, August 22, 2012

ADEBAYOR ATUA TOTTENHAM

Emmanuel Adebayor
Emmanuel Adebayor

Emmanuel Adebayor amekamilisha mipango ya kuhamia Tottenham Hotspur kutoka Manchester City kwa kitita cha pauni milioni 5.
Mshambulizi huyo kutoka Togo alionyesha umahiri wake msimu uliopita, akiichezea Tottenham kwa mkopo, kwa kufunga jumla ya magoli 17 katika ligi kuu ya Premier.

Adebayor atakuwa ni kati ya wachezaji wenye mishahara mikubwa katika klabu hiyo ya uwanja wa White Hart Lane.

Adebayor, mwenye umri wa miaka 28, alikuwa akilipwa na Manchester City pauni milioni 175,000 kwa wiki.

Mshambulizi huyo, ambaye zamani alikuwa akiichezea Arsenal, alifichua habari za kujiunga na Tottenham kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter: “Tottenham niko njiani! Natamani magoli. Kaeni chonjo.”

Mkataba wa Adebayor ulikuwa uendelee kwa miaka miwili zaidi na klabu ya Man City, na kwa kipindi kirefu katika misimu miwili iliyopita alikuwa akiichezea Real Madrid ya Uhispania, na kisha Tottenham.

“Ninafurahi kujiunga kabisa na Spurs baada ya klabu kuelewana na Manchester City,” aliongezea Adebayor.

“Pengine ilichukua muda mrefu kinyume na ilivyotazamiwa, lakini nimefurahi sana kurudi Tottenham Hotspur. Nilifurahi sana nilipokuwa hapa msimu uliopita, na ni matumaini yangu tutaweza kwa pamoja kufanikiwa hata zaidi.”

Inafahamika kwamba Spurs walikataa kubadilisha mipango yao ya mishahara ili kufanikisha mipango ya kumpata Adebayor.

Lakini kutokana na Adebayor kukataa kupunguziwa mshahara, mabingwa wa ligi kuu Manchester City walikubali kuongezea zaidi tofauti ya senti atakazopokea Adebayor katika klabu ya Tottenham, na kiwango alichozoea Man City cha pauni 175,000.

Tottenham watamlipa pauni 80,000 kwa wiki, na Man City ilibidi kukubali kuongezea tofauti ya elfu 95,000 kwa wiki, ili kuyafanikisha makubaliano kati ya vilabu hivyo viwili.

Makubaliano hayo yanahitimisha ubishi ulioendelea kwa muda mrefu, kuhusu ikiwa Adebayor alistahili kulipwa bakshishi na marupurupu mengineyo iwapo angelisisitiza kuondoka Man City pasipo makubaliano kamili kati yake na klabu hiyo.
Mavituz ya Adebayor

Tuesday, August 21, 2012

EVERTON YAIDUNGA MAN UNITED KIMOKO


Fellaini akipiga kichwa kilichozama moja kwa moja kambani kuandika goli la pekee la Everton

Kimuhemuhe cha ligi kuu ya Uingereza kimendelea jana jumatatu huku mamilioni ya mashabiki wa soka duniani wakishuhudia Timu ya Everton ikichabanga Manchester united kwa bakora moja kwa yai katika dimba la Goodison Park, mchezo huo ulishuhudiwa na watazamaji wapatao 38,415.

Katika mtanange huo goli la pekee la Everton lilitupiwa kambani na Fellaini katika dakika ya 56 na kuwaacha hoi Man United.


Cleverley wa Man U akioneshana umwamba na Pienaar wa Everton

Fellaini akishangilia goli

Hapa kazi tuu..Welbeck akiwa chini ya ulinzi mkali


Van Persie akitia mchomo katika mpambano huo

Ngoma ngumu..Rooney na Kagawa wakiwa wameloa baada ya kuchapwa goli la kwanza
 


Daah hivi kweli tumechapwa?

UNAONA UTAAAAAAAMU MAMBO YA BAIKOKO

WAZIRI MKUU ETHIOPIA AAGA DUNIA

Aliekuwa waziri mkuu wa Ethiopia marehemu Meles Zenawi

Waziri mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi amefariki dunia akiwa na umri wa miaka hamsini na saba na ni mmoja wa viongozi wenye ushawishi mkubwa na ambaye utawala wake ulikumbwa na utata barani afrika.
Hali yake ya afya imekuwa ikiangaziwa kwa majuma kadhaa sasa ingawaje hakukuwa na thibitisho kuhusu alichokuwa akiugua hasa.
Taarifa ya baraza la mawaziri imesema kuwa Zenawi alikuwa akipokea matibabu ng'ambo na afya yake ilikuwa ikiimarika lakini akazidiwa siku ya Jumapili alipolazimika kurejeshwa hospitali, ''Ingawaje madaktari wake walifanya kila wawezalo, alifariki jana mwendo wa 23:40,'' taarifa hiyo imesema.
Bwana Zenawi alikuwa kiongozi wa Ethiopia wakati taifa hilo lilipoingia vitani na nchi jirani ya Eritrea mwaka 1998.
Meles Zenawi aliingia mamlakani mwaka 1991 baada ya mapinduzi lakini akapokea sifa kutoka kwa mataifa ya magharibi.
Waziri mkuu wa Kenya raila Odinga ameiambia BBC kuwa ana hofu kuhusu hali nchini Ethiopia kufuatia kifo cha Meles Zenawi.
Alisema kuwa hali nchini humo sio nzuri huku vita vya kikabila vikiendelea kuwa tishio.
Bwana Odinga alimtaja Zenawi kama kiongozi mashuhuri na mwenye elimu bora, aliyejitolea kuunganisha bara la afrika.
Naibu waziri mkuu Hailemariam Desalegn anatarajiwa kuchukua wadhifa huo.

Friday, August 17, 2012

RATIBA KAMILI LIGI KUU UINGEREZA (BARCLAYS PREMIER LEAGUE)

RATIBA YA Barclays Premier League

Mechi zote kwa saa za TANZANIA(EAST AFRICAN TIME)
Saturday 18 August 2012                                                                             
Arsenal v Sunderland Emirates Stadium 17:00
Fulham v Norwich Craven Cottage 17:00
QPR v Swansea Loftus Road Stadium 17:00
Reading v Stoke Madejski Stadium 17:00
West Brom v Liverpool The Hawthorns 17:00
West Ham v Aston Villa Upton Park 17:00
Newcastle v Tottenham Sports Direct Arena 19:30
Sunday 19 August 2012
Wigan v Chelsea The DW Stadium 15:30
Man City v Southampton Etihad Stadium 18:00
Monday 20 August 2012
Everton v Man Utd Goodison Park 22:00
Wednesday 22 August 2012
Chelsea v Reading Stamford Bridge 21:45
Saturday 25 August 2012
Swansea v West Ham Liberty Stadium 14:45
Southampton v Wigan St. Mary's Stadium 17:00
Sunderland v Reading Stadium of Light 17:00
Tottenham v West Brom White Hart Lane 17:00
Norwich v QPR Carrow Road 17:00
Aston Villa v Everton Villa Park 17:00
Man Utd v Fulham Old Trafford 17:00
Chelsea v Newcastle Stamford Bridge 20:30
Sunday 26 August 2012
Stoke v Arsenal Britannia Stadium 15:30
Liverpool v Man City Anfield 18:00

HAYA NDIO "MAJEMBE" YALIYOWAHI KUUZWA NA WENGER


Baada ya Arsenal Wenger kumuuza Mshambuliaji wetu hatari Robin Van Persie kwa mahasimu wetu Manchester United mimi ninajifariji na maneno haya ya Kocha wetu wa kuheshimika zaidi kwetu Arsenal Wenger...lakini roho inaumaaaaa!!

Nafarijika zaidi na maneno ya Arsene Wenger ninapowakumbuka wachezaji mashuhuri na wakaliii aliowahi kuwauza na kamwe yeye hajawahi kununua Nyota katika soka..wapige chapo hapo chini.....

Thienry Henry









Patrick Vieira


Ashley Cole



Samir Nasri

Cesc Fabregas - Arsenal v Stoke City - Premier League
Cesc Fabregas