Friday, June 24, 2011

MANUEL JURADO ATAJWA KUMRITHI CSEC FABREGAS.

Klabu ya AS Roma ya Italy ipo katika mpango wa kumnasa chipukizi wa Barcelona Bojan Krkic kwa kitita cha euro milioni 10. Hii ina maana kwa Barcelona kuweza kutumia pesa hizo na kuongeza zingine ili kumnasa Kiungo wa Arsenal Csec Fabregas. Wenger ili kujiandaa na maisha bila ya Fabregas tayari ameshaweka malengo ya kumnasa kiungo mchezeshaji wa Schalke 04 Juan Manuel Jurado, ambapo mpango wa Wenger ni kutumia paundi za Uingereza milioni 7.5, Jurado aling'ara zaidi katika fainali za ligi ya mabingwa ulaya 2010-2011 ambapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 aliiwezesha Schalke 04 kufika nusu fainali.

No comments:

Post a Comment