Friday, June 24, 2011

MELLO ACHUKIZWA KUBADILISHWA NA MEIRELES

Felipe Mello

Raul Meireles
Kiungo wa Juventus Fellipe Mello amekasirishwa na hafurahii kitendo cha cha uongozi wa Juventus kumtoa "kafara" na pesa kidogo ili kumnasa mchezaji wa Timu ya Liverpool mreno Raul Meireles. Juventus wapo tayari kumtoa Mello na kitita cha paundi za Uingereza milioni 13 ili kumnasa Meireles.Akiwa hajatimiza hata mwaka tangu asajiliwe na Liverpool akitokea Porto kwa ada ya paundi za Uingereza milioni 10,Meireles sasa anahitajiwa na Juventus kwa udi na uvumba. "Kwa hiyo tuseme Juve hawaniheshimu,hicho ndio nachoweza kusema" Mello aliliambia gazeti la Daily Mirror, "Yaani mi si lolote?,mi sio wa kujadiliana kwa bei nafuu" aliongeza Mello.

No comments:

Post a Comment