Friday, August 26, 2011

Tetesi za usajili Majuu zilizotoka hivi punde

Juventus yamuwania Malouda
Mkurugenzi wa Juventus Giussepe Marota ameeleza waziwazi juu ya kumhitaji Malouda katika kikosi chake, kama wakikubaliana watamchukua Malouda mwenye miaka 31 kwa kitita cha paundi za uingereza milioni 5.

Alvaro Perreira kutua Chelsea
Wakati wanatarajia kumuuza Malouda Chelsea wametangaza kuongeza dau kumnasa mchezaji wa Porto ambaye ni raia wa Uruguay Alvaro Perreira, baada ya Porto hapo awali kukataa kitita cha paundi za uingereza milioni 16.6 na sasa wapo tayari kuongeza dau kumnasa Perreira.

Emanuele Giacherini atua Juventus
Juventus imefanikiwa kumnyaka Emanuelle 26, kutoka klabu ya Cesena na hivi sasa yupo Turin akifanyiwa vipimo vya afya.

No comments:

Post a Comment