Tuesday, June 26, 2012

DOGO JANJA AFANYA KUFURU MLIMANI CITY, MANUNUZI MIL 2.5


Abdul Aboubakar Chande "Dogo Janja"

Unaweza usiamini na huenda ukahisi labda ni story za town, lakini ukweli ndio huo, Siku chache baada ya kutua Bongo na Pipa (Ndege) akitokea Kilimanjaro na kujiunga na kampuni ya Mtanashati Entertainments ya jijini, nyota wa Bongo Fleva , Abdul Abubakar Chande ‘Dogo Janja’ mwishoni mwa wiki iliyopita alisomea kisomo maalumu cha kuomba Mwenyezi Mungu amnyooshee mambo yake na "umatemate" zaidi pindi atakapoanza kushusha ngoma mpya.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kisomo hicho kichoshudiwa na Teentz.com, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Ostaz Juma na Musoma alisema kuwa wameamua kumfanyia kisomo hicho kwa lengo la kuweka kazi zote za Dogo janja mikononi mwa Mungu kwa kuwa wanaamini wapo watu ambao hawajafurahishwa na mpango mzima wa dogo huyo kurejea Bongo

Katika shopingi hiyo Dogo janja alitumia zaidi ya shilingi Milioni 2.5 za kibongo kununua vitu mbalimbali, kama Seti 5 za viatu, Suti 4, Jeans 10, T shirt 10,miwani 5, simu aina ya BlackBerry, Laptop na vitu vingine kibao .
Huku akionekana mwenye furaha kubwa Dogo Janja aliiambia Teentz.com kuwa amefuahi kwa kiasi kikubwa kwa yale yote ambayo Ostaz Juma na kundi zima la Mtanashati kwa yote wanayomfanyia hivi sasa kwani hatakuwa na malipo mengine zaidi ya kuwafanyia kazi nzuri zenye kiwango.

“Nina furaha sana, hakika namshukuru Ostaz kwa yote anayofanya kwangu sina la kusema zaidi wasubiri ngoma za kweli zitakazokuwa kama shukurani kwao kwa sababu ndiyo kitu pekee ambacho naweza kukifanya kwao” alisema Dogo Janja.


No comments:

Post a Comment