Tuesday, June 26, 2012

STAR WA BONGO MOVIE FLORA MVUNGI KATIKA KASHFA YA UTAPELI WA 200,000/=


Flora Mvungi

Star maarufu katika tasnia ya filamu za kibongo "Bongo Movies" Flora Mvungi ameshutumiwa kupokea mlungula wa kiasi kadhaa unaofikia shilingi za kibongo laki mbili (200,000) kutoka kwa mtayarishaji wa filamu chipukizi aliejulikana kwa jina moja la Othman.

Akielezea mkasa huo wa "kupigwa" Tshs 200,000/= za kibongo na staa wa filamu nchini Mtayarishaji huyo wa filamu a.k.a Producer amesema Alikubaliana na Flora ampatie kiasi hicho ili aweze kushiriki katika filamu anayoiandaa inayoenda kwa jina la MZIWANDA. Othman anasema walipokubaliana alimtumia Flora mkwanja huo kwa njia ya Tigopesa, lakini ilipofika muda wa kuwa mahala pa kutayarisha filamu (Location) Staa huyo hakutokea kwa visingizio lukuki. Lakini Producer huyo akafunguka kuwa safari hii ilikuwa mara ya nne kuzinguliwa na Flora katika maswala mazima ya kufika eneo la tukio maarufu kama Location.

Producer Othman alipokuwa akihojiwa na kituo kimoja maarufu cha redio hapa nchini alifunguka hayo na ndipo mtangazaji wa kipindi hicho alipoamua kuwaunganisha kwa njia ya simu, katika hali ya mshangao staa huyo alikana kumfahamu Producer huyo wa movie za kibongo lakini alikiri kuwa kuna filamu ambayo aliitwa akashiriki lakini kutokana na sababu fulanifulani hakufika na akaahidi aitwe mambo yatakapokuwa tayari.
Utamu ukanoga pale mtangazaji alipomvutia kamba Flora Mvungi na kisha akamuuliza maswali kadhaa halafu akamuweka hewani wapeane makavu na producer, Hali ilikuwa ya majibizano makali Flora akikana kupokea mkwanja hali iliyoonekana kumkera zaidi Producer huyo na akisisitiza kuwa staa huyo asijifanye mjanja kwani yeye ana uthibitisho wa Message alizomtumia pesa ghafla Flora akakata simu nganjaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!! Hali hii iliacha SINTOFAHAMU ikiwa imetanda katika sakata hilo.

No comments:

Post a Comment