Monday, January 28, 2013

LIVERPOOL TOTTENHAM ZAFUNGASHIWA VIRAGO KOMBE LA FA

Tottenham imebanduliwa nje ya mashindano ya kuwania kombe la FA baada ya kulazwa magoli mawili kwa moja na Leeds United.

Luke Varney aliifungia Leeds bao lake la kwanza kabla ya Ross McCormack, kufunga la pili. Tottenham ambayo inashiriki katika ligi kuu ya Premier nayo ikapata bao lake kupitia kwa mchezaji wake Clint Dempsey.
 



Mtukutu El-Hadji Dioff akishangilia kuibandua Tottenham

Katika mechi nyingine Chelsea, nusura iage mashindano hayo baada ya kulemewa na Bendford.

Hata hivyo Fernando Torres aliifungia Chelsea bao lake la pili na kuiepushia aibu kubwa.

Timu hizo mbili zilitoka sare ya kufungana mabgoli mawili kwa mawili.

Liverpool vile vile, imeondolewa kwenye michuano hiyo ya FA, baada ya kunyukwa magoli 3-2 na Oldham, ambayo inashiriki katika ligi daraja ya kwanza.

Timu zingine za ligi kuu ambazo zimefuzu kwa raundi ijayo ni pamoja na Manchester United, Everton, Arsenal, Wigan, reading na Manchester City.

Norwich, QPR na stoke city zinaungana na timu ambazo zimefunganya virago vyao katika michuano hiyo ya FA.

Wachezaji wa Liverpool hoi baada ya kubanduliwa nje ya kombe la FA na Oldham

Wayaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa


Wachezaji wa Oldham wakishangilia baada ya kuidungua Liverpool

Leeds 2-1 Tottenham
 
 
 
Oldham 3-2 Liverpool
Chelsea 2-2 Brandford

No comments:

Post a Comment