Wednesday, December 19, 2012

MESSI BADO YUPO SANA BARCELONA

Lionel Messi amekubali kusaini mkataba mpya na klabu ya Barcelona, utakaodumu kwa mwaka wa 2018.

Nyota huyo kutoka Argentina, mwenye umri wa miaka 25, amekuwa na miaka minne ya mafanikio na klabu hiyo na pia kwa taifa lake.

Kufikia sasa Messi amefunga jumla ya magoli 90 mwaka huu pekee.

Mlinda langu Carles Puyol, 34, na mcheza kiungo Xavi Hernandez, 32, pia wamesaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Barcelona.

Ripoti zinasema kuwa wachezaji hao sasa watasalia na Barcelona hadi mwaka wa 2016.

Kwa mujibu wa tangazo kutoka kwa klabu hiyo, Puyol, Messi na Xavi wanatarajiwa kusaini mkataba mpya katika muda wa siku chache zijazo.

Afisa mmoja wa klabu hiyo amesema ni jambo la kutia moyo kuona kuwa Barcelona imefanikiwa kudumisha huduma za wachezaji wake nyota.

Kandarasi ya Messi na Barcelona inakamila mwa wa 2016 ili hali kandarasi ya Puyol inamalizika mwaka wa 2013 huku kandarasi ya Xavi inakamilika mwaka wa 2014.


Leonel Messi

HAPPY BIRTHDAY BARBARA AMINA HASSAN

Leo ni siku ya kuzaliwa ya mtangazaji wa Clouds entertainment Group Ltd wa kipindi cha Power Breakfast, Barbara Amina Hassan. Napenda kuchukua nafasi hii kumtakia maisha mema alizaliwa lini ana miaka mingapi kwasasa sitaki umbea mtafute mwenyewe ninachojua amezaliwa siku kama ya leo 19 Dec .......

Tuesday, December 18, 2012

ARSENAL YAIZABA READING 5-2 CARZOLA APIGA HAT-TRICK

Mshambuliaji mahiri wa Uhispania Santi Carzola ametupia kambani mabao matatu"Hat-trick" Arsenal ilipoizaba na kuikandamiza kabisa timu iliyopo mashakani katika ligi ya Reading 5-2 na kuipeleka mpaka nafasi ya 15.

Arsenal wakiwa na kumbukumbu ya kunyanyaswa na Bradford katika kombe la ligi wiki iliyopita walitandaza soka la kuvutia.

"It was important to stay strong and play football. Success comes with playing football," Arsenal manager Arsene Wenger aliiambia Sky Sports. "And it was a very convincing win tonight."

Mjerumani Lucas Podolski ndie aliefungua mlango katika dakika ya 14 likiwa ni goli lake la 5 katika ligi kabla ya Carzola kupiga mbili katika kipindi cha kwanza .

Arsenal sasa ina point 27 tayari imecheza michezo 17,point 2 nyuma ya mahasimu wenzao Tottenham Hotspur na 15 nyuma ya Manchester United. Reading inashikilia mkia ikiwa na pointi 9.

Walcott alipigilia msumari mwingine dakika 8 baadaee pale alipoichachafya ngome ya Reading na kumchambua mlinda mlango Adam Federici.

Dakika ya 32 Podolski alifanya kazi nzuri na kumchungulia Carzola akiingia eneo la hatari na bila ajizi alimpenyezea pasi murua nae bila kupepesa macho akakandamiza mpira wavuni, goli hili ni ushahidi tosha wa ubovu wa safu ya ulinzi ya Reading .

Goli la nne kazi nzuri ya Gibbs kumdodoshea mpira wa kichwa Podolski eneo la hatari nae akamuona Carzola amekaa uzuri na kumuachia pande na Carzola kutupia bao tamu sanaaa.

Dakika ya 14 wakitokea mapumziko Carzola anatupia bao la 3"Hat-trick" shukran za pekee zimuendee Wilshere anaempenzezea pande murua Podolski nae kama kawaida anmsusia ngoma Carzola nae bila kupepesa macho anatupia kambani goli la 5 na la mwisho.

Mara ya mwisho timu hizi kukutana ni katika kombe la ligi Arsenal ikiwa nyuma kwa mabao 4-0 wanarudi mchezoni na kupitia muda wa nyongeza wanaichabanga Reading 4-7.

Le Fondre alifanya kazi nzuri dakika ya 66 alipomhadaa kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny na kuandika bao la kwanza, zikiwa zimesaalia dakika 19 mpira uishe Kebe nae akatupia kambani bao la pili na mpaka mwisho Arsenal 5-2 Reading.
Podolskiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii


Walcoooooooooooooooooooooooooooooooooooootttt


Carzola na wenzake wakishangilia goli

S.Carzola akielekeza mashambulizi langoni mwa Reading



Goooooaaaal, Carzola akifunga goli kwa kichwa


Kocha wa Reading Brian McDemott akiwa haamini kilichotokea


Kocha wa Arsena Arsene Wenger akimpongeza Theo Walcott kwa kazi nzuri aliyoifanya

ARSENAL 5-2 READING

KATONGO MWANASOKA BORA BBC 2012 AWABWAGA DROGBA,YAYA TOURE NA DEMBA BA

Naodha huyo wa Zambia mwenye miaka 30 amemshinda Demba Ba, Didier Drogba, Younes Belhanda na Yahya Toure na kuwa mshindi wa kwanza kutoka Kusini mwa Afrika katika historia ya mashindano hayo.
Orodha ya washindani hao ilitangazwa na wataalamu wa soka Afrika, ambao wamezingatia umahiri wa mchezaji, uwezo wa kiufundi na ushirikiano na wachezaji wengine.


Christopher Katongo akipokea tuzo ya BBC ya mwanasoka bora wa Afrika 2012


Katongo na tuzo ya BBC


Katongo akibusu kombe la mataifa ya Afrika

Na idadi kubwa ya watu wamepiga kura kupitia njia ya mtandao au ujumbe mfupi huku asilimia 40 kati yao wakimchagua Katongo, ambaye anachezea timu ya China Henan Construction.
Katongo ameweka rekodi mpya ukizingatia kwamba wachezaji wote walioorodheshwa katika kinyang'anyiro hicho walikuwa na mwaka wa mafanikio, wanne kati yao walikuwa wameshinda medali mbalimbali, ni Katongo pekee ambaye mafanikio yake yamezingatiwa na mashabiki wa mpira Afrika.

Katongo, ambaye ni mwanajeshi nchini Zambia, alikuwa kivutio pale alipoiongoza Zambia, katika michuano ya kombe la Mataifa Bingwa barani Afrika mnamo mwezi Februari mwaka huu.

Alifunga magoli matatu katika fainali iliyoandaliwa nchini Equatorial Guinea na Gabon na baadaye kufunga bao la ushindi kupitia mkwaju wa penalti na kuisadia Zambia kubeba kombe hilo.

Zambia iliishindi Ivory Coast kwa 8-7 katika fainali hiyo baada ya timu hizo mbili kutoshana nguvu baada ya muda wa kawaida na muda wa ziada mjini Libreville.

MATUMAINI YA ZAMBIA KUELEKEA BRAZIL
Kilikuwa ni kipindi kilichojawa na hisia kwa Zambia, ambayo miaka 19, iliyopita ilipata msiba mkubwa, pale ndege iliyokuwa imebeba wachezaji wa timu ya taifa ilipoanguka mita 500 tu kutoka Libreville, na kuuwa wachezaji wote 25 pamoja na rubani wa ndege hiyo.

Miezi saba baada ya kuoingoza Zambia kushinda kombe hilo, Katongo pia ameng'ara katika michuano ya kufuzu kwa fainali za mwaka ujao,wakati alifunga goli la pekee dhidi ya Uganda.

Bao hilo lilikuwa bao muhimu sana kwa Zambia kwa kuwa ilipoteza mechi iliyofuatia kwa kuchapwa bao moja kwa bila, lakini ikafuzu kwa fainali za mwaka 2013 zitakazofanyika Afrika ya Kusini baada ya kushinda kwa magoli 9-8 kupitia mikwaju ya penalti.

WAJIPANGA KUFUZU KWA FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA
Na zaidi ya hayo yote, Katongo amechangia kwa kiasi kikubwa harakati za kufufua matumaini ya Zambia kufuzu kwa michuano ya kombe la dunia mwaka 2014.

Chris  Katongo
Naodha wa Zambia Chris Katongo

Zambia ililazwa magoli 2-0 na Sudan mjini Khartoum mwezi Juni, matokeo ambayo hadi wakati huu hayajathibitishwa, huku uchunguzi ukiendelea kuhusu hatua ya Sudan ya kumchezesha mchezaji ambaye hakusajiliwa.

Wiki moja baada ya mechi hiyo Zambia ilikipiga na Ghana na Katongo kwa mara nyingine ndiye aliyetupia kambani bao la ushindi na hivyo kuimarisha matumaini yao ya kufuzu.

Ikiwa Christopher Katongo ataendelea kuwa katika kiwango alichonacho kwa sasa, huenda akaisaidia Zambia kupata matokeo mazuri wakati wa michuano ya kuwania kombe la dunia nchini itakayoandaliwa nchini Brazil miezi kumi na minane ijayo.

Katongo katikati akiruka sarakasi kushangilia moja ya magoli yake

Katongo akifanya mambo dimbani
Video Katongo akifanya vituuz graundini

Monday, December 17, 2012

KINA DADA/MAMA FUNGA MWAKA NA STYLE MPYA YA RANGI ZA KUCHA

 


WANYAMA NAO SIKUKUU YA X-MAS INAWAHUSU







































CORINTHIANS YAIDUNGUA CHELSEA FAINALI YA KOMBE LA KLABU BINGWA YA DUNIA

Klabu ya Corrinthians kutoka Brazil, imeibuka kidedea katika michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa duniani baada ya kuidungua Chelsea ya Uingereza kwa bao moja kwa "nunge" katika mechi ya fainali iliyochezwa nchini Japan.
Paolo Guerrero ndie aliepeleka msiba Uingereza akitupia bao la pekee na la ushindi kwa Corinthians.
Hata hivyo Chelsea, ilipoteza bafasi nyingi za kufunga wakati wa mechi hiyo pale washambuliaji wake walipokuwa wakipepesa macho na kutetemeka miguu kutupia kambani pindi wanapofika katika eneo la hatari la Corinthians.
Katika muda wa ziada Fernando Torres, alipoteza nafasi nzuri sana ya kuzawazisa licha ya kuwapiku walinzi wa Corinthians na kubakia yeye na mlinda mlango Cassio alieonekana "mnoko" kwa kuchomoa hatari nyingi zilizoelekezwa langoni mwake ambapo Torres alijaribu kumlamba chenga kipa huyo wa Corinthians na kuachia fataki lakini kombora lake likawa hafifu na kudakwa kwa urahisi na kipa.

Chelsea ilimaliza mechi hiyo ikiwa na wachezaji kumi baada ya Gary Cahil, kupewa kadi nyekundu baada ya kumfanyika madhambi mchezaji wa Corrinthians Emerson.
Bao la chelsea lililofuingwa kwa kichwa na Fernando torres lilikataliwa na hivyo vijana hao kutoka brazil wakaibuka na ushindi.

Paolo Guerrero akitupia bao pekee kwa kichwa katika mpambano huo...mtazame Ramires na Ashley Cole wanatamani waudake lakini waaaapi baaadae sanaaaa!!



Guerrero akishangilia goli huku Ashley Cole akisafisha vyombo kambani na David Luiz akiwa tayari kumsaidia.


Ashley Cole akimthibiti Henrique

Hazard akipata kichapo..hapa braza mawili, mpira ubaki wewe uende au mpira uende wewe ubaki..upo!?


Tulia nimwage majaro weweee...


Aiyaaaaaaah tumekosa!!?? Tulieni nyinyi tumetumwa kombe sisi alaaaaahh


Wachezaji wa Corinthians wakiwashukuru mashabiki kwa support baada ya mtanange kuisha


Inauma sana unajuaa . Nahodha wa Chelsea Frank Lampard akiwa na majonzi ya kulikosa kombe.


Emerson wa Corinthians akimfariji Mbrazil mwenzake Ramires..ndio ukubwa kaka kama vipi rudi home ushangilie makombe.



Kazi tuliyotumwa kutoka Brazil imetimia hureeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!